Tangazo

Tangazo

NEEMA GASPA KUACHIA ALBAMU MPYA YA NI SHUJAA...

Jumapili, 29 Juni 2014

HARUSI YA WAIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI, ROSE MUSHI NA NIKODEMUS SHABOKA JR YAFANA

Duniani wawili wawili, hili limetimia kwa mwimbaji wa nyimbo za Injili Rose Mushi na Nikodemus Shaboka Jr. baada ya kiu yao ya muda mrefu ya kuitwa mume na mke kutimia siku ya leo. Inapendeza kuona watu wanaacha na ukapera wa kushindia chips na sasa kuingia katika ndoa wakiwa na uhakika jioni kuna msosi kamili nyumbani. Ukapera unaumiza sana kwani unakuwa huna ratiba maalumu ya misosi, unaweza ukagonga chips au soda na biskuti ikawa imetoka.

Rose Mushi

Tunamshukuru Mungu kwa kuwasaidia watumishi wa Mungu hawa kwa kuwaunganisha kuwa kitu kimoja. Tunawaombea maisha mema yenye baraka katika ndoa yao hii ambayo imefanyika baraka kwa walio wengi na wanaowajua wanandoa hawa.

Maids

Sasa tunaamini kazi yao ya kumtumikia Mungu itakuwa haina maswali mengi kama ilivykuwa zamani. Rose Mushi mbali na uimbaji pia ni mwandishi wa vitabu na ni mwalimu wa kufundisha mambo mbalimbali. Amekuwa akifundisha hata maswala ya ndoa hata kama yeye alikuwa hajaolewa, Mungu alikuwa akimtumia na kumpa ujasiri wa kujibu hata maswali ambayo pengine yalikuwa yakimhusu kutokana na ukapera wake.

Rose Mushi

Wanandoa hawa wameleata heshima katika kanisa na familia yao. Inapendeza kwa wazazi wanapoona watoto wao wanaolewa na kuoa. Tumekuwa na vijana wengi sana ambao bado hawajaolewa na kuoa, na wanatamani kuoa na kuolewa lakini kuna vitu ambavyo vinawazuia, inawezekana ikawa kifedha, dini, nguvu za giza, woga wa maisha na vitu vingine kama hivyo.

Ewe mwanandoa unapaswa kuwaombea watu kama hawa ili waweze kuishi maisha kama haya ambayo Rose na Nikodemus wanaenda kuishi sasa.

 Rose Mushi na mume wake Nikodemus Shaboka Jr
  Rose Mushi na mume wake Nikodemus Shaboka Jr





 Nickodemus Shaboka Jr. Akiwa na Norman Massawe best man.

FURAHA ISAYA KUFANYA UZINDUZI WA ALBAMU YAKE YA "NITASEMA NDIYO KWA BWANA" LIVE

Inafurahisha kuona sasa vijana wa Yesu wanafanya kazi ya Mungu kwa viwango vingine bila hata ya kuogopa changamoto zinazowazunguka. Hii tunasema ni kuthubutu bila ya kuangalia nani anasema nini, bali ni kumuangalia Jehova.

Furaha Isaya ni mwimbaji wa nyimbo za injili ambaye kwa sasa Mungu amemuweka katika viwango vingine vya kimuziki. Mungu ameweza kumsaidia na kumuwezesha kumaliza albamu yake ya NITASEMA NDIYO KWA BWANA" akiwa amewashilikisha baadhi ya waimbaji kama vile John Shabani.

Mungu hakuishia hapo, pia amempa kibali cha kuweza kuzindua albamu yake LIVE katika ukumbi wa URAFIKI SOCIAL HALL ulipo Sinza Legho. Tamasha hili litaanza saa 6 mchana hadi saa 12 jioni na kutakuwa na kiingilio cha Tshs. 2,000 tu.

Tamasha hili limegubikwa na waimbaji wengi sana, baadhi yao ni Atosha Kissava, Ambwene Mwasongwe, Madam Ruti, Edson Mwasabwite, Neema Gasper, Masanja Mkandamizaji, Sarah Mvungi, Joshua Makondeko, Mercy Kitundu, Mess Chengula, Stella Joel, Emmanuel Mabisa, Grace Rwegasha, Enock Jonas, Marry Mgogo, Silas Mbise, Julieth Dougras, John Shabani, Jerry Mtumishi, Hondwa Mathias, Petro, Emmanuel Peter, Danniel Safari, Leah Amos, Margreth Sembuche, n.k

DON MOEN KUSHEREKEA MIAKA 40 YA NDOA YAKE

Wow! I’m sitting here in St. Thomas, USVI reading over all the wonderful greetings and blessings from friends all over the world. My heart is touched deeply! And, I receive all of your many blessings and kind words! Yes, God has been so faithful!
Several of you have asked how it all began, so I thought I’d respond briefly. Laura and I got married May 19th, 1973 after a concert in Minneapolis, Minnesota. We had been touring South Africa and Europe for 12 months prior to that. Laura was a nanny to Evangelist Terry Law’s 8 month old girl (Misty) and our team photographer! We had met at Oral Roberts University two years earlier in April 1971. It was love at first sight (at least for me!). It took Laura a little longer!! Ha!!
I toured for the next year with a singing group, Living Sound, while Laura remained at ORU. After her semester ended in May 1972, I asked her to come travel with our group on the road for a couple of weeks so we could be together. While she was visiting me, she began to take care of Terry and Jan Law’s little baby girl, and when it came time for her to leave, Terry and Jan asked her if she’d be willing to stay for the year and take care of the baby while Jan sang. I was thrilled!! My girlfriend was going to be traveling with me throughout Europe and Southern Africa! ☺
I proposed to Laura in April 1973, in Johannesburg South Africa at the end of our tour there. I sold my bass guitar (a beautiful 1963 Fender Jazz Bass) and bought our rings, the same ones we are wearing today! We returned to the USA in May with Living Sound to begin a tour of the churches that supported our missionary trip, which included a two day stop (Saturday and Sunday) in Minneapolis. The church met at a beautiful old theater on 14th and Nicollet Avenue.

Don Moen na mrs

Laura and I were married after our concert Saturday night. After the concert, Terry Law told the audience, “Following the concert tonight you’re all invited to stay for the wedding of our guitarist, Don Moen and his fiancĂ©, Laura Shrock.” The wedding started at 10:00 PM and I had a thousand people at my wedding that I didn’t know!! ☺ The entire Living Sound group sang at my wedding and I played “Love Is A Many Splendored Thing” on my violin as Laura walked down the aisle. She was beautiful! The church was kind enough to provide cake, punch and coffee for all the guests, and my buddy Joe Anderson was kind enough to take some pictures. Laura bought her dress on sale for $85 and someone graciously paid for our stay at the Ramada Inn for our honeymoon. Our entire wedding cost $350!!!
While the group sang on Sunday, Laura and I were given the day off, and we were back on the road staying in people’s homes on Tuesday! People would ask us how long we’d been married and you should have seen the look on their faces when we told them “2 days”!!! We just kept traveling, and haven’t really stopped except to have 5 children in between. What a fabulous journey! Yes there have been challenges but through it all, we have found that God is faithful! Here’s to the next 40 years Babe!!

Mtoto wa Don, John na kipenzi chake Sarah
You might also like:

Ijumaa, 27 Juni 2014

VUNJIKA MBAVU NA KING MAJUTO NDANI YA FILAMU YA INSIDE

Filamu hii Jennifer Kyaka (Odama) ambayo inayonyesha maisha ya wafanyakazi maofisi wanaovyofanya vituko na mabosi wao na wengine hata kumkufuru na kumuudhi Mungu kwa vitendo vya rushwa na uvivu kazini, kwa mana Mungu amesema asiyefanya kazi na asile. Watu badala ya kufanya kazi wanabaki kupiga stori na majungu maofisi. Wadada wanavyotumia uzuri wao kuwalaghai waume za watu kwa kutoa rushwa ya ngono. Hakika kama mcha Mungu ndani ya hii filamu utajifunza mengi na utaburudika na vituko vya wasanii maarufu wa kuchekesha kama KING MAJUTO na  BENY, pia utamuona marehemu RACHEL HAULE, DAVINA, ODAMA, DULLAH WA PLANET BONGO, na wengine wemgi sana. Filamu hii ambayo imetengezwa na kampuni bora Tanzania ya J-FILM 4 LIFE itakuweka mahali fulani KIMAWAZO.


VIONGOZI WA DINI WAJA VIKALI JUU YA STAA WA BONGO MUVI J. WOLPER KUBADILIBADILI DINI


Stori:Gladness Mallya

TABIA ya staa wa filamu za Kibongo, Jacqueline Wolper kubadilibadili dini mara kwa mara imeonekana kuwakera watu mbalimbali akiwemo Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Musa Salum ambaye amemcharukia vikali.


Staa wa filamu za Kibongo, Jacqueline Wolper akipozi.

Wolper kiimani ni Mkristo lakini hivi karibuni alibadili na kuwa Muislam kabla ya kurejea tena kwenye imani yake ya awali ya ukristo.

Sababu ya Wolper kubadili dini ilikuwa ni kufunga ndoa na aliyekuwa mchumba wake Abdallah Mtoro ‘Dalas’, walipoachana akaamua kurudi kwenye ukristo.

Akizungumza na Risasi Jumamosi juzikati, Shehe Salum, alisema Wolper anapaswa kujichunguza na kubadilika haraka kwani kitendo anachofanya ni kinyume na taratibu za dini.
“Siyo vizuri hata kidogo na hata dini zote zinakemea kitendo cha kuchezeachezea dini kwani ni chukizo kwa Mungu.


Jacqueline Wolper akiwa kazini.

“Kwa upande wa Dini ya Kiislamu, kuna sheria kali zaidi kwa mtu akionekana na tabia hiyo, anaweza hata kuuawa hivyo wanaofanya mchezo huo waache kwani siyo vizuri. Huko ni kumfanyia Mungu dhihaka,” alisema Shehe Salum na kuongeza:

“Unajua suala la imani ni kitu kinachomhusu mtu binafsi, ni vyema kufanya uamuzi wa hakika na kushika njia moja na siyo kufanya dhihaka na dini ya Mwenyezi Mungu. Ni kitu kibaya sana.”
Naye Juma Suleiman, mkazi wa Ilala, jijini Dar es Salaam alimwambia mwandishi wetu kuwa, katika imani ya kiislam kunakatazwa watu kucheza na dini huku akisisitiza anayefanya hivyo anaweza kulaaniwa.

“Dini siyo kitu cha kuchezea, ni daraja la kumfikisha mtu kwenye haki, si mahala pa kuingia na kutoka, kuingia na kutoka. Huko ni kucheza na Mungu. Namshauri huyo mtoto (akimaanisha Wolper) abadilike. Asifanye mchezo na imani, Mungu anaweza kumlaani kwa kumchezea,” alisema Suleiman.

KWA MSAADA WA MUNGU MWANAMKE AJIFUNGUA BAADA YA KUWA MJAMZITO KWA MIAKA 14


Mwanamke wa Nigeria aliyejitambulisha kwa jina la Mercy James amesimulia tukio la ajabu la kujifungua salama mtoto wa kike baada ya kuwa mjamzito kwa kipindi cha miaka 14. Mtoto aliyeamua kumuita ‘Miracle’
Kwa mujibu wa Vanguard, Mercy alieleza kuwa alianza kujisikia dalili za ujauzito miaka 14 iliyopita lakini awali dalili hizo zilikuwa zinabadilika na mara nyingine anaingia katika hedhi kwa siku moja, lakini hali ilianza kuwa serious miaka miwili baadae alipoenda hospitali na kuhakikishiwa kwa vipimo kuwa ni mjamzito.
“Nilienda tena kwa tabibu miaka miwili baadae na kumlalamikia kuhusu maumivu niliyokuwa nayapata, aliniambia tena kuwa sina tatizo la tumbo na kwamba huo ulikuwa ujauzito. Alinishauri niendelee na maombi ili Mungu aniepushe na mikono ya shetani.” Mercy alisimulia.
Anaeleza kuwa alikuwa anatumia madawa mengi ya kutibu magonjwa ya tumbo lakini hali yake haikubadilika.

Hali iliendelea hivyo hadi ilipofika June 7 mwaka huu ambapo alienda tena katika hospitali hiyo akiwa analalamika na kusikia kila dalili za kitu kutaka kutoka mwilini mwake, lakini hakufahamu kuwa hiyo ingekuwa siku ambayo angejifungua mwanae wa kike, ‘Miracle’.
“Kisha Mungu aliamua kunifuta machozi. Katika siku niliyojifungua mwanangu wa kike, mwanzo nilihisi ni minyoo inataka kutoka kwenye mwili wangu bila kufahamu kuwa yule alikuwa mtoto. Hivi ndivyo nilivyomwambia mkunga. Lakini baada ya kunipima alianza kuniambia nisukume. Nilimpotezea. Baadae nikaishiwa fahamu kama dakika 15 na nilipopata fahamu, nilisikia mtoto Analia. Nilishangaa sana na kuchanganyikiwa nilipomuona mwanangu. Sikuweza kuamini macho yangu.” Mercy aliendelea kusimulia tukio hilo.

Naye tabibu wa hospitali ya kanisa la ‘Celestial Church Of Christ, Parokia ya Kadoso ambapo Mercy alijifungulia, aliyetajwa kwa jina la Ajegunle aliliambia Vanguard kuhusu hatua zote alizopitia hadi kujifungua mwanae huyo na jinsi yeye binafsi kama mkunga alivyohusika.
Marafiki na ndugu wa mwanamke huyo walitoa ushuhuda pia kwa gazeti la Vanguard la Nigeria kuhusu tukio hilo la kushangaza. Comment Kiistaarabu Matusi na Kumchafua Mtu Hairuhusiwi

MWIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI DAVID ROBERT NDANI YA BERLIN

Kazi imeanza kwa mtumishi wa Mungu ambaye amepata neema ya kudondoka ndani ya Berlin. Hii ni changamoto kwetu sisi kuona mwimbaji kama huyu anapata channel za ulaya. Ninaamini ukiwa chini ya miguu ya Baba yetu wa mbinguni siku moja atakuweka mahali ambapo hukutegemea kufika.
Lakini jitihada zako pia zinahitajika, juhudi zako za kutimiza ndoto zako zikiwa kubwa ndipo milango ya mafanikio pia inafunguka. Tuzidi kuwa mwaaminifu mbele za Mungu na tusichanganye ya duniani na ya mbinguni kama shortcut ya mafanikio.
Muulize Mungu wako nini amekiweka ndani yako kwa kazi yake ili uanze kukitumia sasa. David aliona uimbaji kwake ni karama aliyopewa na Mungu na ndio maana akakaza buti na sasa anakaa na ngozi nyeupe akichangia maoni yake. Jikubali na sema ninaweza.
 David Robert
 David Robert akiwa ametulia katika jopo la wazungu

MWIMBAJI MUNISHI FAUSTIN ATOA ONYO KWA WATU WANAOTAKA KUMPELEKA ASKOFU KITONGA MAHAKAMANI


Askofu Kitonga

http://www.gospelgtv.com/munishiraisawa.jpg
Faustin Munishi

MFULULIZO WA MBEYA GOSPEL FESTIVAL: ANN ANNIE, RACHEL, MESS JACOB CHENGULA NA WAIMBAJI WENGINE WATIKISA MBEYA

Chama cha Muziki wa Injili Tanzania kiliandaa tamasha linaloenda kwa jina la Mbeya Gospel Festival likiwa na lengo la kuwataka wana Mbeya kujiunga na chama hicho kwaajili ya kuwasaidia kujua haki zao za kimuziki.

Katika tamasha hili kulikuwa na waimbaji wengi sana kama vile Mess Jacob Chengula, Ann Annie, Rachel, na wengine wengi. Watu walibarikiwa sana.
 Kutoka kulia ni Rachel, Ann Annie
 Rachel Sharp kutoka Sweden
 Emmanuel Mabisa
 Mess jacob Chengula mwenye koti jeupe
Ann Annie

MSANII WA BONGO FLEVA NA BONGO MOVIE BABY MADAHA AMGEUKIA MWENYEZI MUNGU

Kufuatia vifo vya wasanii vilivyotokea mfululizo, mwigizaji Baby Joseph Madaha amelazimika kubadili mtindo wake wa maisha na kuishi kitakatifu.
Baby Joseph Madaha

Akipiga stori na wana habari, Baby Madaha alisema anawasihi hata wasanii wenzake wabadili mfumo wa maisha kwa kumgeukia Mungu na kufanya ibada kila mara kwa kuwa vifo hivyo vinawapa somo la kuwakumbusha kumkaribia Mungu.

“Nimebadili mfumo wa maisha kwa kufanya ibada na ninawashauri wasanii wenzangu tumgeukie Mungu kwani vifo na mambo yanayotokea yanatukumbusha ibada na kujiweka safi,” alisema Baby Madaha.

MUNGU awasaidie hawa wanaojiona kuwa ni watu maarufu maana umaarufu wao ni hapa hapa duniani, mbinguni hakuna anaowajua. Wanazidiwa umaarufu na watoto wadogo ila tu wanaisha maisha ya kumpendeza MUNGU huku wamempa BWANA YESU maisha yao.

Sio mpaka matatizo yaje ndio tumkumbuke MUNGU lakini wakati wa amani tunamsahau MUNGU kama yupo.

WOKOVU NI SASA NA KAMA SIO SASA BASI NI SASA HIVI.

MZEE WA KANISA ANASWA LIVE GESTI NA BINTI CHINI YA MIAKA 18...MATUKIO KATIKA PICHA



Mzee wa kanisa la kiroho (jina linahifadhiwa kwa sasa), aliyetajwa kwa jina la Luca Pesa, mkazi wa Segerea, Dar, ameaibika baada ya kukurupushwa kwenye nyumba ya kulala wageni (gesti) akidaiwa kutaka kuvunja amri ya sita na binti ambaye ni msanii chipukizi wa filamu za Kibongo, Debora Jacob, Ijumaa lina kisanga cha aina yake.


Mzee wa kanisa la kiroho aliyetajwa kwa jina la Luca Pesa,

HABARI KAMILI
Tukio hilo ambalo kamwe Luca hawezi kulisahahu maishani mwake, lilijiri kwenye gesti hiyo iliyopo karibu na Kituo Kikuu cha Mabasi cha Segerea, Dar, Jumanne iliyopita huku mzee huyo akishushiwa tuhuma nzito ya rushwa ya ngono kwa vibinti chini ya miaka 18.
Katika tukio hilo, mzee huyo wa kanisa na msanii huyo wa Kundi la Maigizo la Vivif lenye maskani yake maeneo hayo walikuwa wamejichimbia kwenye gesti hiyo katika chumba ambacho mlangoni kilikuwa kimeandikwa Rombo kabla ya kuchomolewa na kufikishwa kanisani kisha polisi.

TUHUMA NZITO
Timu ya Oparesheni Fichua Maovu (OFM) ya Global Publishers, ikiwa kwenye mingo zake, ilipokea simu kutoka kwa dada aliyejitambulisha kwa jina moja la Diana na kujieleza kuwa anatoka kundi la sanaa za maigizo la Vivif lililopo Segerea jijini Dar.
OFM: Ndiyo hujakosea unazungumza na
OFM, tukusaidie nini?
Diana: Kuna mzee wa kanisa la kiroho la (anataja jina la kanisa hilo) lililopo maeneo ya Segerea, aliomba kuwa mfadhili wa kundi letu.

Akiwa kwenye geti la kanisa.

Tulimkubalia na baada ya muda alianza kutumia fedha zake vibaya kwa kufanya vitendo visivyofaa.
OFM: Vitendo gani visivyofaa?
Diana: Anawarubuni mabinti wadogo anawaweka kambini na kula nao tunda tamtam eti ndiyo tiketi ya kuchezeshwa kwenye maigizo.
OFM: Tiririka!
Diana: Yaani hadi muda huu ninapozungumza na ninyi mzee huyo wa kanisa anachati na msanii mwingine wa kundi hilo. Anaitwa Debora anataka waende kwenye gesti fulani wakanogeshane, wahini tayari mtego umewekwa utafyatuka muda wowote.

UDHALILISHWAJI?
Diana alisema baada ya Debora kuombwa ‘mambo’ ndipo akawataarifu wasanii wenzake na kuwataka wote kwa pamoja waungane kuikomesha tabia hiyo chafu ya Luca anayelichafua kanisa la kiroho na kulidhalilisha kundi lao la sanaa.

OFM MZIGONI
Baada ya kuseti kila kitu, Diana aliiomba OFM iambatane nao kwani muda huo tayari Debora alishatangulia kwenye gesti hiyo kumfuata mzee huyo wa kanisa ambaye alishachukua chumba.

.....akitaitiwa.

Taarifa hiyo ilipokelewa kwa mikono miwili na kiongozi wa OFM ambaye aliwaagiza vijana wake makini ambao walisitisha kazi nyingine za kiintelijensia kisha kuelekeza nguvu zao eneo la tukio.
Vijana hao walitumia pikipiki zao ziendazo kasi ambapo baada ya muda usiozidi dakika ishirini walikuwa wamefika kwenye gesti hiyo.

ENEO LA TUKIO
OFM walipofika eneo la tukio, walikuta kundi la wasanii hao wakimchomoa gesti mzee huyo wa kanisa ambaye aliruka ukuta na kudondokea kwenye matuta ya viazi.
Akiwa anajizoazoa kwenye matuta hayo, kundi la wasanii hao lilimuunganishia ambapo kabla ya kumnasa aliingia kwenye chumba cha nyumba iliyopo jirani na gesti hiyo ili kujisalimisha.
Hata hivyo, zoezi lake lilifeli baada ya wasanii hao kumtahadhalisha mwenye nyumba hiyo kuwa wanamtaka mtuhumiwa wao la sivyo wangeichoma moto.
Baada ya kuzingirwa na wasanii hao huku akihatarisha maisha yake kwa kuwa wasanii hao walikuwa na hasira, aliona yasiwe makuu akaamua kuwaruhusu wamtoe mtuhumiwa wao wakamalizane naye kanisani.

KABANG!
Alipotiwa mikononi, mzee huyo wa kanisa aliomba apelekwe kanisani ambapo hapakuwa mbali na eneo la tukio ili akahifadhi vitu vyake muhimu pamoja na kuomba ushauri.

APELEKWA MSOBEMSOBE KANISANI
Kundi hilo la wasanii lilimpeleka kanisani msobemsobe ambapo baada ya hatua kadhaa polisi walitokea na kuwadhibiti wananchi wenye hasira na wasanii waliotaka kumdhuru mzee huyo wa kanisa wakati akipelekwa kanisani.

Mtuhumiwa akitembezwa mtaani.

MTAANI WERAAA!
Wakiwa mitaani, njiani mabinti walikuwa wakipiga kelele ‘weraaa…ukomeee…’ huku wakifurahia kufunga mitaa kwa madai kwamba mzee huyo wa kanisa alizidi.
Katika sekeseke hilo, polisi hao walimtia pingu mzee huyo wa kanisa na kuongoza safari ya kuelekea kanisani.
Wakiwa kanisani hapo polisi walijitambulisha na kuwauliza wachungaji pamoja na waumini wa kanisa hilo kama walimfahamu mzee huyo wa kanisa.

BREKI YA KWANZA POLISI
Kundi la wazee pamoja na vijana wa kanisa hilo walikiri kuwa Luca ni mmoja wa wazee wa kanisa hilo ndipo polisi hao wakamruhusu kuwakabidhi baadhi ya vitu vyake ikiwemo simu na fedha kisha breki ya kwanza ikawa Kituo cha Polisi cha Tabata-Shule ambapo alifunguliwa jalada la kesi namba RB/3843/2014 -RUSHWA YA NGONO, KUWAWEKA KAMBI KINYUME CHA SHERIA WASICHANA WENYE UMRI CHINI YA MIAKA 18 NA KUWADHALILISHA KIJINSIA.
Hadi OFM wanaanua jamvi kituoni hapo kanisa lilikuwa likihaha kumchomoa kwa dhamana akisubiri sheria kuchukua mkondo wake.

Alhamisi, 26 Juni 2014

MAREHEMU SHEILA (RACHEL) HAULE NDANI YA FILAMU MPYA YA INSIDE ITAKAYOKUJIA KUANZIA JULAI 13.2014

Ile filamu iliyokuwa ikisubiriwa na Watanzania wengi ya INSIDE ya Jennifer Kyaka (Odama) itakuwepo sokoni 10.07.2014. Filamu hii ambayo imechezwa katika  mazingira ya ofisini ikionyesha vituko vinavyofanyika maofisi na wafanyakazi na pia mabosi. Kama kawaida ya kampuni ya J-Film 4 Life ndio iliyohusika katika kutengeneza filamu hii ambayo ukiangalia utavutiwa na kujua mengi kuhusiana na vituko vya vinatokea  maofisini
Ndani ya filamu hii kuna vituko vya ajabu ukisingatia yumo Majuto, Beny, Dullah, marehemu Rachel Haule, Odama na wengine wengi kama unavyoona katika cover. Jipange mtu wangu kujipatia hii nakala ambayo mpya upate kuongeza siku zako za kuishi kwa kicheko.

MWIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI GRACE RWEGASHA AOMBA MSAADA KUTOKANA NA JINA LAKE KUTUMIA VIBAYA KATIKA FACEBOOK

Grace Rwegasha mabye ni mwimbaji wa nyimbo za injili ameombwa msaada kwa Watanzania wote kumsaidia kutatua tatizo lililomkumba la watu kutumia jina lake katika facebook kuweka picha mbaya yaani picha za ngono. Amesema hawa watu wanalengo la kuchafua huduma yake na jina lake kwa ujumla. Na hivi ndivyo alivyoandika katika facebook account yake:
Grace Rwegasha

NDUGU WAPENDWA KATIKA BWANA, NAWASALIMU KWA JINA LA BWANA WETU YESU KRISTO. KWA WALE RAFIKI ZANGU MNAOPENDA KUWASILIAN A NAMI , TAFADHALI HAKIKISHA JINA LANGU KWA USAHIHI, KWANI KUNA WATU , WANAOJIUNGA NA FACEBOOK KWA KUTUMIA JINA LANGU KWA KUONGEZA HERUFI MOJA KATIKA JINA. KWA HARAKAHARAKA WAWEZA FIKIRI NI JINA LANGU KUMBE SIO NA HABARI WANAZOWEKA KATIKA PAGE HIZO NI MBAYA.. NDUGU WAPENDWA NAOMBA MNISAIDIE KATIKA HILI. MBARIKIWE SANA.

HATIMAYE MCH. DEBORA SAID AZIKWA NA MAELFU YA WATANZANIA SIKU YA JUMATATU 23.06.2014 JIJINI DAR ES SALAAM

Mchungaji na mwimbaji wa nyimbo za injili Tanzania Debora Said amekuwa dunia tangia mwaka 1972 na mwaka huu wa 2014 Juni Mungu amemchukua kwa mapenzi mema. Mch.Debora Said amefanya kazi yake akiwa duniani, amewaleta watu wengi kwa Yesu kwa njia ya uimbaji na uchungaji wake, ameisaidia familia yake mbali na huduma yake ya uimbaji na uchungaji.
Katika sherehe hii ya kumuaga Mch. Debora Said kulikuwa na waimbaji weng0i sana, baadhi yao ni Upendo Nkone, Victor Aron, Joshua Makondeko, Chidumule, Neema Gasper, Madam Ruti, Lungu la Yesu, Addo November, Christina Matai, Miriam Lukindo, Chriss, Martha Mwaipaja, Kyambiki, Petro, Apostle Gideon Mutalemwa, Upendo Kilahiro, na wengine wengi sana.

Askofu John Said mume wa marehemu Mch. Debora Said
Siku hii ilikuwa ni siku ya furaha na shangwe kwa kumuaga mtumishi wa Mungu Debora Said, waimbaji waliweza kuimba kwa furaha na bila kuonyesha huzuni. Lakini haikuishia hapobali watu wengine walionekana wakitoa machozi na kulia kwa sauti, na hii inaonysha ni jinsi gani Mchungaji  Debora Said alikuwa mchango mkubwa Tanzania na Afrika nzima.
Katika sherehe hii kulihudhuriwa na wachungaji wengi sana kwaajili ya kumuaga mpendwa wetu Mch. Debora Said. Wachungaji waliweza kutoa maneno machache kukuhisiana na msiba huu na wengine walionekana wakishindwa kujikaza na badala yake machozi yakiwatoka.

Rulea Sanga aliyekaa na shart nyeusi akitafakari
Tunamshukuru sana Mungu kwa kumpa ujasiri mume wake na marehemu Askofu John Said, alionekana ni mtu mwenye ujasiri kwa sura na akiwa na matumaini ya kwamba mke wake ametwaliwa na Mungu wetu wa mbinguni. Kibinadamu inaumiza sana kuona yule uliyekuwa unamtegemea kimawazo ametoweka duniani. Hakika huu ni wakati mugumu sana kwa Askofu John Said na kanisa lake zima kwa maana wameondokewa na mtu ambaye alikuwa kama nguzo ya kanisa.

Kwa wasiojua, ni kwamba marehemu Mchungaji Debora Saidi alikuwa ni mwimbaji, Mchungaji na pia mwanamichezo (netball). Kutoakana na taarifa tulizopata msibani ni kwamba alijituma sana katika ujuenzi wa kanisa lao na pia alikuwa muhimizaji mkubwa katika swala zima la michezo.


Rais wa Chama cha Muziki wa Injili Tanzania, Addo November aliwaomba waimbaji wa nyimbo za Injili Tanzania waache tabia ya kujiona mastaa na kujitenga na wengine wakati wa raha na shida. Alisema anayeweza kukuweka wewe kuonekana staa ni Yesu Kristo tu na sio mwanadamu, Mungu anaweza kukushusha na kumuinua mtu mwingine kwa kazi yake. Pia aliwataka wasijifananishe na watu wa Bongo Fleva kwani wao ustaa mara nyingi wanategemea votes za mashabiki na asilimia kubwa hawategemea kutoka kwa Yesu Kristo. Rais aliwashukuru waimbakji wote kwa usirikiano wao katika zoezi zima la kumuaga mtumishi wa Mungu Mch. Debora Saidi.

Mch mama Fednandes wa kanisa la AGAPE alitoa ofa ya kurusha matukio ya msiba huu wote katika kipindi cha FIRE katika television cha ATN  na pia ameandaa tamasha kubwa la waimbaji wa nyimbo za Injili Tanzania hapo kanisani kwake.
KIPINDI CHA KUPELEKA MWILI WA MAREHEMU MCH. DEBORA SAID KANISANI
Wa pili kutoka kushoto ni Askofu John Said mume wa Marehemu Mch. Debora Said akijianda kuingia Kanisani

WAIMBAJI WAKISHREKEA SIKU YA PEKEE YA KUMUAGA MWIMBAJI MWEZAO MCH. DEBORA SAID
 Tumaini Njole akimsindikiza rafiki yake Mch. Debora Saidi

Edson Mwasabwite akisema bye bye Debora Said huku akiimba wimbo wa Ni kwa Neema tu
MC Joshua Makondeko

Kwaya ya kanisa la Maisha ya Ushindi kwa Askofu John Said

Waimbaji kutoka Chama cha Muziki wa Injili Tanzania (CHAMUITA) wakiimba wimbo maalum wa kumuaga mpendwa wao marehemu Debora Saidi


Edson Mwasabwite

Neema Gasper (aliyeshika mic)

Apostle Gideon Mutalemwa

 Christina Matai hakuweza kujizuia, alijishtukia analia wakati waimbaji wenzake wakiimba. Hii inaonyesha ni jinsi gani alipigwa na kifo cha marehemu Mch. Debora Said

 Sifa John
Kutoka kulia ni Victor Aron

Upendo Nkone


Lungu la Yesu


Mchunga Anton Lusekelo (Mzee wa Upako)
Mchungaji Anton Lusekelo "Mzee wa Upako" (aliyekaa)
 Mwimbaji wa nyimbo za injili Petro aliyevalia koti la draft
 wa kwanza kutoka kwenye nguzo ya kanisa ni mume wa Upendo Kilahiro
wa pili kutoka kushoto mstari wa kwanza ni mwimbaji Orida Njole

Mume wa Martha Mwaipaja (kulia) akiwa na mke wa Mtume Fidnandes wa ATN



Mchungaji Harisi Kapiga

MATUKIO MBALIMBALI YAKIENDELEA NJE YA KANISA WAKATI SHEREHE IKIENDELEA KANISANI


 Victor Aron (mwenye tshirt nyeusi akiwa na baadhi ya marafiki wakibadilishana mawazo
 Baadhi ya waimbaji walioamua kupiga picha ya kumbukumbu


 MC Joshua Makondeko mwenye kitamba cha bendera ya taifa akiwaelekeza wenzake ratiba ya waimbaji
 Miriam Lukindo (kushoto.gauni nyeusi) na kulia ni Tumaini Njole
Mwimbaji wa Gospel Tanzania Furaha Isaya (kulia)

 Gideon Mutalemwa akichukua namba za simu kutoka kwa mtumishi wa Mungu Datson

 Sarah Mvungi akifanya mawasilia

KIPINDI CHA KUOMBEA CHAKULA


 Upendo Kilahiro (wa pili kutoka kulia) akiongea na rafiki yake





KIPINDI CHA KUTAMBULISHA WACHUNGAJI NA WAGENI MBALIMBALI



 Wachungaji, mitume na viongozi mbalimbali (waliosimama)
Waliosimama ni wake wa wachungaji
"Nyamayao" wa tatu kutoka kushoto
 Bloga na mtangazaji wa WAPO REDIO Silas Mbise akifanya kazi ya Mungu

 Mchungaji Mama Finandesi wa ATN akisema jambo
Askofu John Said akiwa na mwanae

 Rais wa Chama Cha Muziki Tanzania (CHAMUITA) Addo November akiwashukuru waimbaji kwa kujitolea kufika katika msiba huu. Pia aliweza kusema waimbaji waache kujiita mastaa kwa anayekupa ustaa ni Yesu Kristo na sio mtu mwingine. Leo unaweza kuonekana unang'aa lakini kesho Mungu akamuinua mtu mwingine.

ASKOFU JOHN SAID AKIWA AMEMKARIBISHA MAMA HUYU KUSEMA JAMBO KUHUSIANA NA KIFO CHA MKE WAKE
Mama huyu alionekana kulia wakati wote hata ulipofika wakati wa kula chakula bado alionekana kulia huku akila chakula. Mama huyu alishikwa na uchungu mkubwa kwa kutwaliwa kwa marehemu Debora Said
 Kulia ni Askofu John Said
Askofu  John Said

 KIPINDI CHA KUOMBEA WATU WALIOWEZA KUOKOKA SIKU YA MAZISHI YA MCH. DEBORA SAID

Picha zimepigwa na Rumafrica
www.rumaafrica.blogspot.com

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...