Tangazo

Tangazo

NEEMA GASPA KUACHIA ALBAMU MPYA YA NI SHUJAA...

Jumanne, 23 Julai 2013

SHUHUDA ZA JUMAPILI YA 21.07.2013 KATIKA KANISA LA YESU KRISTO LA HUDUMA YA MAOMBEZI NA UPONYAJI

Dada kutoka Kenya ambaye ni muathirika wa UKIMWI alifika kwa Nabii Flora kwaajili ya maombezi ya uponyaji. Dada huyu alisema alivutiwa sana na ushuhuda wa Miss Kanda Mashariki Tanzania, Martha Julius ambaye alikuwa na virusi vya UKIMWI na baada ya kuhangaika sana aliweza kufika kwa Nabii Flora na akaombewa na mwisho wa siku akapona.


Dada kutoka Kenya akiwa na Nabii Flora
 Kulia ni mshindi wa Miss Kanda Mashariki Tanzania Martha aliyepona UKIMWI akimfariji dada kutoka Kenya ambaye alimuona kwa kupitia facebook na akafunga safari kutoka Kenya akiwa na imani kuwa akifika kwa Nabii Flora atapata Uponyaji. Jumapili hii Nabii Flora aliweza kumuombea
 Dada kutoka Kenya haamini kumuona rafiki yake aliyepona UKIMWI na yeye anatamani kupona UKIMWI na anaamini Nabii Flora kwa nguvu za Mungu atamponya
Hawa wote unawaona wameathirika wakifarijiana kwa kumkumbatia dada aliyepona virusi vya UKIMWI Martha Julius
EVANS KUTOKA MOSHI APONA FIGO
Bwana Yesu asifiwe, Kwa jina ninaitwa Evans nimetokea Moshi, nilikuja kwa Nabii Flora siku ya Alhamisi nikiwa na hali mbali sana. Lakini sasa hivi ninaona Mungu amenisaidia ninaendelea vizuri. Kipindi nakuja hapa nilikuwa sitembei nimebebwa katika kiti. Tatizo hili nilikuwa nalo tangia mwaka jana (2012) kutokana na figo zangu kuoza na moyo wangu ulilika sana.
Mke wake alikuwa na haya ya kusema: Jamani mimi ninamshukuru sana nabii Flora alivyomtendea mume wangu (baba Evans).Mnamo mwezi huu wa sita kulekea wa saba, mdogo wake aliongozana na mume wangu kuja Dar es Salaam kwaajili ya vipimo. Shemeji yangu akanambia ninaamini kaka yangu atapona akifanyiwa maombi, nikamuuliza ni kanisa hgani? Akanambia wewe twende nitakuonyesha kanisa. Nikamwambia kwasababu baba Evans anaumwa sana ngoja tupunguze maji. Kweli mdogo wake na baba Evans akaja hapa na mume wangu na alipofika hapa akawa ni mtu wa 19 kwa wale wanaotakiwa kumuona nabii Flora.
Tulipofika hapa kanisani, baba Evans alisumbua sana, alikuwa haoni, hana nguvu ni mtu wa kushikiria. Tilipofika Nabii akasema wenye matatizo wapiti mbele ili waombewe hasa wafanyakazi (na sisi tukajichanganya humo humo). Tukamkarisha baba Evans katika kiti. Nabii Flora aliposogea tukamnyanyua. Nabii Flora akamshika mkono na akamuombea. Baada ya kumaliza kumuombea akamwambia, “Nimekwambia tembea’’ Mara tukaona baba Evans anatembea taratibu taratibu na jinsi anavyoendelea kutembea, mabadiliko yanatokea na kuwa mazuri.
Ulipofika wakatii wa kumuona nabii Flora, watu walitupisha na tukaonana naye. Nabii alipomuona akasema huyu mtu ameoza ini, ameoza figo na moyo, kwahiyo anatakiwa abomolewe. Nabii akamuombea kwa danu ya Yesu. Jana tulienda kupima hospitalini, kwa kweli mambo ni mazuri sana. Nabii Flora ametusaidia bila ya malipo yoyote. Sina kitu cha kukurudishia Nabii Flora ila Mungu ataendelea kukulinda
MAJI YA UPAKO YAVUTA KILIO CHA GETRUDE BAADA YA WANAE KUTESWA NA WAPANGAJI.
Bwana Yesu apewe sifa, mimi ninaitwa Getrude Gelvasi Magingo, ninakaa Mbagala Dar es Salaam Tanzania. Mwezi wa 9 mwaka 2013 nilihamia kwenye nyumba ambapo nilipata matatizo makubwa sana. Baba mwenye nyumba ambaye anakaa mkoa wa Mtwara alikuwa akilalamika na kodi ya wapangaji amabao walikuwa hawalipi nay eye anategemea hiyo kodi kuendesha maisha yake.. Kipindi anazungumza hayo mimi nilikuwa nimesafiri. Wapangaji wenzangu wakawa wanawambia wale wanangu kuhusu kodi, wakawa wanawapiga na kuwamwagia chakula.
Nilipopigiwa simu jinsi wanangu wanavyoteseka ilibidi nirudi na nilipofika Ubungo, Dar es Salaam nikaja moja kwa moja kanisani kwa nabii Flora, nikalala na asubuhi ilipofika Nabii Flora aliombea maji yangu. Nilienda nyumbani na nilipofika wanangu wakanieleza matatizo yaliyotokea. Mungu akasikia kilio change, wale wapangaji wawili waliokuwa wakisumbua familia yangu juzi wamehama.
Muda si mrefu nikapata simu kutoka kwa mwenye nyumba kuwa anahitaji nimpeleke kwa nabii Flora ili amuombee kwani ana matatizo yanayomsumbua.
Ninamshukuru sana Nabii Flora.
KIJANA KUTOKA MWANZA APONA KANSA NA BABA YAKE MKUBWA, PROFESA MOROGORO APONA UPOFU
Bwana Yesu asifiwe, mimi ninatokea Mwanza Bugando na jina langu ni Edstamus Thomas na ni mwanafunzi kidato cga sita. Nilikuwa na tatizo la jicho la kansa tokea nimezaliwa. Nilienda kupima Bugando wakanambia ni kansa. Nikaambiwa matibabu ya kansa yanapatikana katika hospitali Ocean Road Dar es Salaam kwa njia ya mionzi. Tuliandikiwa referal letter Mwanza kuwa twende Dar es Salaam.
Tulipofika Dar es Salaam, ilibidi tuanzie Muhimbili katika hospitali ya Rufaa. Madaktari Muhimbili waliangalia jicho langu na kuniambia niende baada ya wiki mbili. Mama akanambia twende kwenye maombi kwa Nabii Flora, kwa muda wa wiki mbili hizi Mungu atatenda.
Nilipofika hapa kanisani nilionana na Nabii Flora na akanambia nitapona. Na ukumbuke hospitalini walinambia ninatakiwa kufanyiwa operation ya kuondoa jicho. Basi tukawa tunakuja hapa kanisani na baba mkubwa ambaye ni profesa Morogoro ambaye alikuwa na tatizo la kutoona (kipofu). Alipokuwa akihudhuriwa maombi aliweza kupona na sasa anaona. Na mimi nimeweza kupokea uponyaji nimeambiwa sina kansa kabisa.
Mama wa huyu kijana alikuwa na haya ya kusema: Baada ya wiki mbili kuishi tukaenda tena hospitalini na wakatuambia maendeleo ni mazuri na tuendelea kutumia dawa ndani ya wiki moja. Wiki moja ikiwa bado haijaisha tukawa tumepigiwa simu kwamba, aende wakaamwangalie tena hospitalini ili wapate ufumbuzi ili arudi shuleni. Ndipo tukaamua kuja kwa nabii Flora na kuweza kumuombea, na baada ya kumuombea na kufuta jicho la mwanangu kwa kitambaa na kurudisha jicho ndani. Tulipoenda siku ya Ijumaa, madakatari wakamwamngalia wakasema, hii sio kansa ila ni tatizo linguine, kwahiyo inabidi tuendelee kwa miezi mitatu, baada ya hiyo miezi mitatu kuisha turudi hospitalini na kuangalia maendeleo yake na ndipo tutakapowaruhusu.
ALISHA MUSA ALIYEPONA UKIMWI YEYE NA MWANAE NA MUME WAKE AMSHUKURU NABII FLORA KWA MAENDELEO MAZURI YA MAMA YAKE ANAYEUMWA.
Bwana asifiwe. Kwa jina ninaitwa Alisha Musa, Mungu amenitendea mengi sana. Nilikuwa na HIV nilipona kwa kupitia Nabii Flora. Kuna jambo ambalo sitasahau ambalo Nabii Flora alilisema ya kwamba, “Tuchukue kitambaa cheupe” nilichukua kile kitambaa na sikujua kuwa mama yangu ataumwa. Niliondoka na vile vitambaa viwili, kimoja nikampa mwanangu na kimoja nikawa nacho. Baada ya wiki moja nikapigiwa simu na kuniambia mama yako anaumwa sana na amelazwa hospitali. Nikamwambia mama yangu utapona na mimi niko njia ninakuja huko Moshi. Nilipofika nikakuta mama yangu anakula kwa kutumia mpira na kukojoa kwa kutumia mpira. Nikachukua maji niliyoondoka nayo hapa kanisani na nikampapasa nayo usoni. Nilimpigia Nabii Flora na akaniombea. Mama yangu alikuwa anakoroma tu, ana ameteseka kwa muda wa wiki mbili. Nikasema “Eh Mungu wa nabii Flora, ninaamini, kama mimi nilipona UKIMWI na mtoto wangu na mume wangu, basin a mama yangu hatakoroma tena”. Mama yangu ikabidi wampeleke hospitali nyingine na alipofika kule wakasema mama huyu hana ugonjwa wowote. Tukaondoka na kumpeleka KCMC, na pale hakuweza kupokea uponyaji wake. Mama yangu ikabidi arudishwe nyumbani. Nikampigia simu Nabii Flora na nikamwambia mama yangu anaongea lakini anaongea kwa shida sana. Na mpaka sasa ninaongea mandeleo yake ni mazuri lakini mkono wake mmoja haufanyi kazi.
BIBI SILVIA MBUYA AMSHUKURU MUNGU KWA MWANAE KUJIFUNGU SALAMA
Bwana Yesu asifiwe. Ninaitwa silvia Mbuya. Ninashukuru sana madhabahu hii ya Nabii Flora. Nilimpigia simu mwanangu alikuwa na mimba ambayo imepitiliza siku zake na kufikia miezi 10. Ilibidi afanyiwe oparesheni na bahati nzuri Mungu akaona hilo na hawajaweza kumfanyia operation na amejifungua salama.
Mwanangu tangia amejifungua amelazwa hospitali Muhimbili kwa muda wa wiki moja sasa. Ninamshukuru Mungu anaendelea vizuri sana.
Pia eneo ninalokaa nimezungukwa na wachawi na watoto wangu wanalia sana usiku, na mimi ninaota ndoto mbaya sana.
Ninakushuru sana Nabii Flora
DADA AMBAYE ALIFNGWA KIMASOMO AKITAMANI KWENDA KUSOMA ULAYA, NDOTO YAKE YATIMIA
Bwana Yesu asifiwe, kwa jina ninaitwa Samason, nilikuja hapa kanisani, nikaonana na Nabii Flora Peter nikamwambia ninataka kwenda Ulaya na chuo maendeleo yangu sio mazuri. Akanambia Ulaya utaenda na ninakuona umefungwa. Baada ya kununifanyia deliverance, nilipofika chuo nikawa ninaendelea vizuri, nimemaliza masomo yangu salama, na nimepata chuo ninaenda Hungary. Ninamshukuru sana Nabii Flora.
MWANAFUNZI APONA ALEJI ILIYOMSABABISHIA KUSHINDWA KUFIKA SHULE, SASA ASHIKA NAMBA MOJA DARASANI
Bwana Yesu asifiwe, kwa jina ninaitwa Maolela. Ninamshukuru Mungu wa nabii Flora ameniponya. Nilikuwa nasumbuliwa na aleji upele kwa muda wa miaka mitatu hata shule nilikuwa ninashindwa kwenda. Wanafunzi wenzangu wakawa wananicheka wakisema labda nina UKIMWI. Wazazi wangu wote walifariki. Lakini nilipofika mahali hapa Mungu ameniponya, na sasa ninaendelea vizuri na masomo, ninafaulu vizuri sana, ninamshukuru sana Mungu wa Nabii Flora kwani hata namba moja ninashika darasani.
VUMI APONA UVIMBE WA TITI, AOKOTA FEDHA MPAKA KUFIKIA TSH. 50,000
Kwa jina ninaitwa Vumi Lamson Kahama. Mimi ninapenda kumshukuru Mungu wa Nabii Flora. Jumapili iliyopita nilikuwa nasumbuliwa na ziwa langu, nilivimba sana kupita maelezo (jipu), nilishindwa hata kushika mtoto na waumini walikuwa wakinisaidia kushika mtoto. Baada ya ibada nikaonana na Nabii Flora akaweza kulishika ziwa langu na kuliombea, akasema ikifika saa 12 jioni ninaamuru uvimbe huu na uishe. Ilipofika saa 12 niliweza kumshika mtoto na zuwa likapungua uvimbe, likabaki na uvimbe kidogo. Siku ya Jumatano nikaja na kumueleza tena nabii Flora, akashika titi langu na akasema ninaamuru hili buya lote liishe na uishi kwa amani.
Ninamshukuru sana Mungu wa Nabii Flora amenitendea miuujiza.
Muujiza wa pili: Jamani tangia nije katika kanisa hili ni mwezi wa 6. Jumapili ya kwanza nikasali mahali hapa, Jumapili ya pili nilipokuja hapa nabii Flora alikuwa akifundisha jinsi ya kupokea mwezi wa Eludi (6). Nabii Flora akaombea maji yangu, nilipotoka hapa nikasema sifiki nyumbani lazima nifike katika Showbiz yangu nimwagie maji. Baada ya kumwagia maji. Baada ya hapoa niakapanga vitnavyotakiwa kupangwa na nikaacha kijana wangu akiendelea na kazi. Nilipotoka hapoa nikaanza kuokota fedha, nikaokota 500, 1000, 5000, 10000 mpaka zikafika 50,000/= Kwa kweli nilitetemeka sana nilishindwa kuelewa, nilijua ni Mungu wa Nabii Flora ndiye anayeonyesha miujiza hii. Hakika Mungu wa nabii Flora anaweza.
MAMA MZAZI WA MARY SHEMILA AWEZA KUTEMBEA MUHIMBILI ALIKOLAZWA
Bwana Yesu asifiwe, kwa jina jninaitwa Mary shemila, nimesimama hapa kwa niaba ya mama yangu Mary shemila ambaye amelazwa katika hospitali ya Muhimbili Dar es Salaam toka tarehe 8. Jumapili iliyopita nilikuja hapa nikamuona mtumishi wa Mungu Nabii Flora. Mama yangu alikuwa hawezi kutembea kabisa. Lakini baada ya mtumishi Nabii Flora kumuombea, mama yangu aliweza kutembea.
Nabii Flora alituomba katikati ya wiki tumlete mama yetu, lakini masharti ya pale Muhimbili ni magumu sana, hatukuweza kupata nafasi ya kumleta. Sasa leo tumeweza kupata nafasi na tumemleta tena mama yetu ili Nabii Flora akaweze kumuona tena. Asante Mungu.
ROBERT AFUNGULIWA MAJINI ALIYOTUPIWA. YEYE NA UKOO MZIMA
Mimi ninaitwa Robert Mwaipoa, ni mwenyeji wa Mbeya ila kwa sasa ninaishi Bunju. Mimi nilitupiwa nguvu za kishirikina katika ukoo. Tulikuwa na majini na vifaa vya aina mbalimbali. Nimezunguka mapaka nikaenda kwa waganga.
Nilipokutana na mpendwa mmoja akanambia unahangaika nini, yupo mganga wa waganga katika kanisa la Yesu Kristo kwa nabii Flora. Nikamwambia unicholee ramani na mimi nitafika mwenyewe. Nilipoelekezwa nikawa nimekosea kidogo na kuingia kanisani moja jirani na hili. Baada ya kupotea nikachukua pikipiki na kufika hapa kwa nabii Flora nikajua hapa upo uponyaji.
Ulipofika wakati wa kuombewa, niliombewa na baada ya hapo nikajisikia nimefunguliwa. Ulipofika wakati wa kumuona Nabii Flora kesho yake jioni, akasema hilo tatizo lako ni dogo, lete maji yaombewe. Nilipokunywa yale maji nilitapika sana. Baada ya kuona hayo ndio maana leo nimekuja kwa ushindi mkubwa wa uponyaji.
DADA ALIYEVUNJIKA MKONO BAADA YA MAOMBEZI MKONO UMEPONA
Bwana Yesu asifiwe, mimi nilikuja juzi mkono wangu ilikuwa umevunjika, baada ya kufika hapa mkono wangu umepona. Mkono wangu ulikuwa umefungwa bandeji
R.WILSON KALEBELWA ALIYEKUWA AKIFELI MITIHANI APATA MUUJIZA WA KWENDA CHUONI KUSOMA
Bwana asifiwe, kwa jina ninaitwa R. Wilson Kalebelwa, ninamshukuru Mungu wa madhabahu hii amenifungua. Nilikuwa mwanafunzi niliyekata tamaa kutokana na kufeli sana kimasomo. Lakini kwa kupitia madhabahu hii ya Nabii Fllora, Mungu amenifungua nimemaliza shule, na majibu yangu nimepata na ilibidi niondoke leo kuelekea chuoni. Mtumishi Nabii Flora alisema nisiondoke leo bali ondoka kesho Jumatatu. Ninamshukuru sana Mungu.
DADA  APONA UKIMWI BAADA YA KUOMBEWA NA NABII FLORA PETER


MAMA NA MWANAE WAPONA UKIMWI BAADA YA KUOMBEWA NA NABII FLORA PETER


DADA APONA UKIMWI BAADA YA KUOMBEWA NA NABII FLORA PETER

DADA APATA MUUJIZA WA KUJENGA NYUMBA BAADA YA KUOMBEWA NA NABII FLORA PETER

BABA APONA KISUKARI BAADA YA KUOMBEWA NA NABII FLORA PETER

TIKETI ZA TAMASHA LA UZINDUZI WA ALBAMU YA SHUJAA YA NEEMA GASPA ZINAPATIKANA SASA


Mambo yameiva sasa katika tamasha la kihistoria la uzinduzi wa albamu ya Shujaa ambalo litasindikizwa na waimbaji wakubwa Tanzania. Tumeona matamasha lakini hili ni kiboko ya yote. Ukihitaji tiketi wasiliana na namba hizo katika tangazo.

Tangazo limetengenezwa na RUMAAFRICA
+255 715 851523

Ijumaa, 19 Julai 2013

MWINJILISTI SARA MVUNGI AKISHUKURU WALE WOTE WALIOMUOMBEA NA KUMFARIJI KATIKA MSIBA WA BABA YAKE-TANGA

Sara Mvungi

Wapendwa nawapenda saawote ambao mumeniombea faraja na wale wote ambao mumenitumia pole,neno langu ni hili NAWAPENDA WOTEmumekuwa na mimi katika kipindi hiki kigumu sana sana kwangu jamani ni kipindi kigumu sana,nisema asante kwa yeyote aliyenitumia rambi rambi kwa maneno hata kwa mchango MUNGU awabariki amen love you

NEEMA GASPA ATAHUDUMU KATIKA SEMINA ILIYOANDALIWA NA MCHUNGAJI JOYCE MUTALEMWA



Mwimbaji wa Nyimbo za Injili amesema na Rumafrica ya kuwa leo atakuwa anahudumu katika Semina iliyoaandaliwa na Mchungaji Joyce Mutalemwa katika maeneo ya Moroco hapa jijini Dar es Salaam kuanzia saa 8:00 mchana na kuendelea.

Neema Gaspa

Kumbuka ya kuwa Neema Gaspa anatarajia kuzindua albamu yake ya inayoenda kwa jina la SHUJAA katika ukumbi wa UBUNGO PLAZA tarehe 01.09.2013. Katika tamasha hili kutakuwa na mgeni rasmi Mh. Samwel Sitta. Pia kutakuwa na waimbaji kama Rose Muhando, Evelyn, Ambwene Mwasongwe, Bahati Bukuku, Enock wa Zungukazunguka, Apostle Gideon Mutalemwa, Mwanamapinduzi, Martha Mwaipaja na wengine wengi.

Kiingilio kwa watoto ni Tshs. 2,000, Viti vya kawaida Tshs. 5,000 na VIP ni Tshs. 10,000
Wote Mnakaribishwa

kwa maelezo zaidi tembelea www.neemagaspaa.blogspot.com

Jumatatu, 15 Julai 2013

ALBAMU YA SHUJAA ANAZIDI KUAANGWA NA VIUNGO VITAMU TAYARI KUZINDULIWA UBUNGO PLAZA


Tumeona matamasha mengi sana, tumeona waimbaji wengi sana, tumebarikiwa sana na uimbaji, tumeona watu wenye vipaja na karama za ajabu sana hapa duniani. Lakini hujawahi kuona hiki ambacho Mungu amekiweka kwa mwimbaji huyu wa nyimbo za injili Tanzania Neema Gaspa.

Umefika wakati wangu na wewe kufurahi na kubarikiwa na ujumbe moto moto kutoka kwa Neema Gaspa. Yaani sipati picha UBUNGO PLAZA patakuwaje siku ya 01/09/2013 mida ya saa 7:00 mchana. Kwa haraka haraka kuna watumishi wa Mungu watakaomsindikiza Neema Gaspa, baadhi yao ni kama Rose Muhando, Bahati Bukuku, Ambwene Mwasongwe, Evelyn, Enock Jonas wa Zungukazungua ,na wengine weng. Kwa kweli hapatakalika

Mtapata kumuona na mzee wa matukio (Paparazi la Yesu) kutoka Rumafrica likiwa busy na kurusha matukio LIVE katika mitandao

SHUHUDA MOTO MOTO KUTOKA KATIKA KANISA LA YESU KRISTO LA HUDUMA YA MAOMBEZI NA UPONYAJI KWA NABII FLORA PETER


Tunamshukuru sana Mungu kwa matendo amkuu anayofanya katika kanisa hili kwa kupitia mtumishi wake mpakwa mafuta Nabii Flora Peter. Mungu amekuwa akifanya makuu kwa watu wake wanaofika hapa kanisani na kuombewa na Nabii Flora. Nabii Flora amekuwa akiwakilisha shida za watu kwa Yesu Kristo na Yesu amekuwa akijidhihirisha kwa vitendo.



Katika shuhuda za Jumapili ya tarehe 7.7.2013 ambayo ni siku aliyozaliwa nabii Flora utapata kusikia juu:

1. Kupona UKIMWI
2. Mtoto aliyepotea kuppatikana
3.Mtoto aliyekufa akutana na baba yake maeneo ya Tandika Yombo.
4.kaka kuponywa kidonda kilichomsumbua kwa muda mrefu.
5. Watu kupata fedha na kulipa madeni yao
6. Aliyekuwa kichaa na kuvua nguo, sasa amemaliza masomo yake na ana masters.
7. Aliyekuwa hashiki mimba sasa ajifungua mtoto.
8. Aliyekuwa Miss Kanda Mashariki apona UKIMWI
Na shuhuda nyingi utaziapata

Baadhi ya watakaoshuhudia

MAMA  ALIYEKUWA ANATAFUTA MTOTO APATA MIMBA
Bwana Yesu asifiwe; mimi nilikuja hapa nilikuwa na tatizo la kutokushika mimba, nikamweleza Nabii baada ya maombi ya Nabii nikapewa siku 21 nitakuwa ninamimba. Na kweli zilipotimia siku 21 nimeenda kupima nimekutwa nina mimba, namshukuru sana Mungu.



 MISS KANDA YA MASHARIKI-TANZANIA, MARTHA JULIUS APONA UKIMWI
Bwana Yesu asifiwe, mimi naitwa Martha Julius, nilikuwa miss kanda mashariki (mkoa wa Morogoro, mkoa wa Pwani, na mkoa wa Dar es Salaam) 2004/005 na nilikuwa mshindi namba moja, na hii ilinisababishia kuingia katika mashindano ya miss Tanzania 2004/2005. Mimi kabla sijaja hapa kwa Nabii Flora niligundulika mwaka 2010 kuwa nina HIV. Baada ya hapo nikaanza kuhangaika kutafuta tiba. Niliposikia Loliondo kuna uponyaji nilienda bila ya mafanikio,  baadae nikasikia kuna mtoto anaitwa Subira yuko Masasi na huyo mtoto ni wa miaka 8 au 9 anaponyesha magonjwa yote. Ukishuka Masasi kumfikia huyo mtoto lazima ulipie pikipiki shilingi 20,000. Nilienda kwa yule mtoto na nikakaa wiki mbili nikitumia dawa zake, lakini sikuweza kupona.Ikabidi nirudi hapa Dar es Salaama na nikajiunga na kanisa ambalo sitaweza kutaja jina, nikahudhuria maombi lakini sikupata uponyaji. Siku moja nikaona habari za nabii Flora katika mtandao, ninakaamua kuja hapa kwa nabii Flora.


Jamini nimehangaika sana, na nimepoteza fedha nyingi sana, kwa maana kila unapokwenda kutafuta dawa za kuponya UKIMWI lazima uende na shilingi 500,000. Kwa mfano Loliondo tulienda na shilingi 300,000 kwa mtu mmoja, Mtwara nimeenda mara mbili na shilingi 300,000 na nilitakiwa kukaa huko kwa muda wa wiki mbili  na nijitegemee malazi na kila kitu. Kuna watu wengine wapo hapa dar es Salaam kama watu au watano ambao nao nimekuwa nikiwaendea na sikuweza kupata mafanikio.


Ninapenda kumshukuru Mungu wa madhabahu hii, nilipokuja ilikuwa ni siku ya Jumapili asubuhi na nilionana na nabii Flora nikamweleza kuwa mimi ninaumwa HIV, na nabii akanitabiria kuwa nitapona na nihudhurie siku 21, kweli nikaudhuria siku 21 na siku ya Ijumaa iliyopita ndio nilitimiza siku 21. Nikaja kwa Nabii Flora na nabii akaniambie niende nikapime kama nimepona au sijapona. Nikamwambia nabii ninaomba niongezee siku 7 za ziada, lakini nabii akanambia nimekuambia nenda ukapime na majibu yawe mabaya au mazuri ninaomba wewe uniletee.

Mchungaji Jury akisoma cheti cha Elizabeth Julius kinachoonyesha hana HIV

Ninamshukuru sana nabii Flora kwani tangia nimefika mahali hapa na kupokea uponyaji, sikuweza kutozwa kitu chochote. Ninamshukuru sana nabii Flora kwani nilipofika hapa na kumueleza shida yangu alinisihi sana kuhudhuria maombi, na akasema, siku nikikosa nauli yeye atanipa nauli. Nabii amekuwa akinipa nauli na ikiiisha naenda kwake na ananisaidia 10,000/=. Pia rafiki zangu kama Jack na Catherine wamekuwa wakinisaidia nauli sana, na mapaka nimemaliza siku zanggu 21 na maombi.
Kwa kweli nikuwa na hofu sana kwenda kupima ikapidi niwachukue marafiki zangu Jack na Catherine ili wanisindikize.

Rafiki zake walikuwa na haya ya kusema juu ya Martha Julius:

Jack (kulia) akishuhudia juu ya rafiki yake Miss Kanda Mashariki 2004/2005,Martha Julius alipona UKIMWI

Jack: Bwana asifiwe, kwa jina ninaitwa Jack, rafiki yake na Martha, na Catherine, tuliamua kwenda St. Mary Kawe kupima, lakini Martha akawa anakata kwani alikuwa haamini kuwa amepona. Tulipofika pale akachukuliwa damu na tukasubiri dakika 15, baada ya dakika 15 akaitwa na alipoitwa daktari akampa majibu na kumwambia sasa uko NEGATIVE. Ilikuwa ngumu sana kwa Martha kuamini. Kabla ya kupima, tukiwa kanisani katika maombi tulikuwa tukimwambia achilia moyo wako kwa Mungu na Mungu wa nabii Flora atafanya miujiza, naye alifanya hivyo na kweli amepkea na sasa ni mzima.

APONA UKIMWI BAADA YA KUAMINI KUWA KWA KUPITIA MTUMISHI WA MUNGU NABII FLORA ATAPONA
Bwana Yesu asifiwe, Ninamshukuru Mungu kwani amenitendea makuu katika madhabahu hii. Nilianza kuja hapa mwezi uliopita (Juni) mwanzoni nikiwa na HIV POSITIVE. Kabla ya kuja hapa kanisani kwa nabii Flora baada ya kungundulika nina POSITIVE, nilikuwa s0ina amani, nilikuwa sipati usingizi mzuri, saa tano usiku uzingizi unakuwa umekwisha.

Nilikuja baadaye kukumbuka kuwa kuna mtumishi wa Mungu anaitwa Nabii Flora na kabla ya kuhamia Mbezi Salasala alikuwa Maguruwe. Kipindi hicho cha nyuma kabla sijawa na HIV niilikuwa siamini kuwa Nabii Flora anaweza kutibu UKIMWI, lakini yaliponikuta ikabidi niamini.

Nilikuja hapa kanisani na kuonana na nabii Flora na kumueleza matatizo yangu, naye aliniambia nihudhurie Jumapili nne. Nikajaa Jumapili ya kwanza na ya pili na  wiki ya kukaribia Jumapili yan tatu, siku ya Jumatano nikaja. Nikamweleza Nabii Flora kuwa nimekuja na tatizo langu la HIV lile la HIV, na pia nina malaria na Typhoid. Nabii akanambia nenda Jumamosi ukapime. Ninkamwambia Nabii bado sijafikisha mwezi mmoja kama ulivyosema kwaza nina wiki mbili. Nabii akanambia wewe nenda kapime na jibu utakalo likuta njoo nalo, na jibu likwa Negative au Positive wewe njoo mimi nitajua nikutibu vipi. Siku ya Jumamosi nikaenda hospitali ya kwanza Mwananyamala nikakuta Neagative, nikawa siamini, nika mwambia daktari kuwa kuna majibu umeficha na sio hayo, daktari akanambia yeye yuko kazini kwahiyo ahawezi kudanganya.

Nikaenda hospitali ya pili Kijitonyama, na nilipofika nikaambiwa Negative. Nikampigia simu Nabii Flora. Nimepokea muujiza wangu kabla ya siku 21 hazijafika. Ninamshukuru sana Mungu wa Nabii Flora Peter.

Nabii Flora alikuwa na haya ya kusema: Alipokuja kijana huyu siku ya Jumatano ya wiki ya tatu. Mungu akwa amekuja usiku akanambia ninakuletea watu machoni pako, na aliponiletea watu hawa, nikamuona huyu kijana. Siku ya Jumatano ilipofika nikamwambia Nenda ukapime na umeshapona.
BABA ALIYEKUWA NA KIDONDA KISICHOPONA SASA AMEPONA
Bwana Yesu asifiwe, kwa jina naitwa Joseph; mimi nilikuja hapa  nilikuwa na kidonda kisichopona kwa muda mrefu, nimezunguka sana bila mafanikio lakini baada ya maombi ya Nabii Flora sasa nimepona, namshukuru sana Mungu wa mahali hapa.


BINTI ALIYEKUWA ANAUMWA NA MENO SASA AMEPONA
Bwana Yesu asifiwe, naitwa Tumaini; mimi nilikuja hapa nilikuwa na tatizo la meno, meno yalikuwa yaniuma sana hata nashindwa kutafuna andazi, lakini baada ya kuleta dawa ya meno hapa Nabii akaiombea sasa nimepona na ninakula kila kitu. Namshukuru sana Mungu.


MTOTO ALIYEKUWA ANAUMWA SASA AMEPONA BAADA YA KUNYWA MAJI
Bwana Yesu asifiwe; kunamtoto wa mwenye nyumba wetu alikuwa anaumwa sana, sasa mimi kunamaji  ambayo Nabii alikuwa ameyaombea hapa Kanisana, baada ya kumpelekea akanywa Yule mtoto akanyanyuka na akaanza kuongea wakati alikuwa hawezi  hata kuongea.


MTOTO ALIYEKUWA AMEPOTEA SASA AMEPATIKANA
Bwana Yesu asifiwe; mimi nimekuja kutoa shuhuda hapa mtoto wangu alikuwa amepote, lakini baada ya kuja madhabahu hii na kuombewa sasa mwanangu nimempata  kama Nabii alivyonitabiria kuwa mwangu yupo na nitampata, namshukuru sana Mungu.


MTOTO ALIYEPOTEA SASA AMEPATIKANA
Bwana Yesu asifiwe; mimi mwanangu alikuwa amepotea kwa muda wa wiki tatu, lakini baada ya kufika mahali hapa na kuombewa mwanangu nimempata kama Nabii alivyonitabiria. Na pia wakati tunarudi nyumbani mtoto huyu alisimama katikati ya barabara wakati kuna roli kubwa lilikuwa linakuja kwa mwendo wa kasi akasema boranife kuliko kuendelea kuishi, lakini kwa nguvu za Mungu lile gari liliweza kuchuna breki. Namshukuru sana Mungu kwa muujiz wake.


MSANII WA BONGO MOVIE  ALIYEKUWA APATI KAZI SASA AMEPATA
Bwana Yesu asifiwe; mimi ni msanii wa bongo move, nilikuja hapa nikamweleza Nabii kuwa toka mwaka umeanza sijaitwa nikafanye kazi, lakini baada ya maombi ya Nabii juzi nikapigiwa simu na msanii mwenza ananiita nikafanye kazi. Kwa kweli namshukuru Mungu pia nimechaguliwa kuwa kiongozi wa kile kikundi.



MAMA ALIYEZURUMIWA NYUMBA SASA IMERUDI
Bwana Yesu asifiwe; mimi nilikuwa na matatizo katika ndoa yangu lakini, mume wangu alinifukuza tukiwa na nyumba mbili na akaoa mwanamke mwingine lakini baada ya kuja hapa kwa Nabii Flora na kuombewa juzi mwanaume ananipigia simu ananiambia nikachukue nyumba yangu inamtesa. Nabii aliniambia kuwa hawatalala mpaka wamerudisha haki yako. Na kabla ya kesi kuisha wamerudisha nyumba. Namshukuru sana Mungu.
DADA ALIYEKUWA HAPATI WATEJA WA I MAZIWA SASA ANAUZA SI KAWAIDA
Bwana Yesu asifiwe, kwa jina naitwa Angle; mimi nina biashara yangu ya maziwa lakini kwa siku nilikuwa nauza nusu lita au siuzi kabisa, lakini baada ya kuja hapa kwa Nabii Flora na kuombewa  nimepata tenda na  nauza lita 30 hadi 50. Namshukuru sana Mungu.

MAMA ALIYEKUWA ANAUMWA NA KIFUA SASA AMEPONA
Bwana Yesu asifiwe, naitwa Hawa; mimi ni muhumini mahali hapa, juzi siku ya ijumaa nilikuwa naumwa na kifua kilikuwa kimenibana sana na ninashindwa kuhema, nikamuomba Nabii Flora naye akaniombea kwa muda wa dakika chache, baada 8ya kuombewa nilijisikia wepesi, kifua kilichokuwa kimenibana kikaachia na mafua yakaachia. Kifua change kuuma kilianza siku nyingi tangia mwaka 1997, nimetibiwa Kiroboto nikaambiwa nina pumu, nikachekiwa Muhimbili nikaambiwa  nikaambiwa nina pumu. Juzi nilipokuwa nikienda Moshi barabra ilikuwa chafu sana. Pumu yangu ilikuwa ikianza lazima nikachome sindano za mshipa lakini baada ya kuombewa sasa  ni mzima na sijachoma tena zile sindano  na ninaendelea vizuri kabisa.Ninamshukuru sana Mungu.


MTOTO ALIYEKUWA  ANAUMWA ALMONIA  SASA AMEPONA
Bwana Yesu asifiwe; nilikuja hapa mwanangu alikuwa anaumwa na Almonia kila siku, uso wake ulikuwa umevimba na akawa amebadirika uso wake na kuwa mweupe, lakini baada ya kuombewa na Nabii Flora namshukuru Mungu mwangu amepona na mpaka sasa anaendelea vizuri, Mungu ambariki sana mtumishi wake Nabii Flora.


DADA ALIYEKUWA APEWI PESA YA MATUMIZI NA MUME WAKE SASA ANAPEWA
Bwana Yesu asifiwe; mimi baba watoto wangu alikuwa amenitelekeza anipi matumizi ya watoto, lakini baada ya kuombewa na Nabii Flora sasa anatoa matumizi na nyumbani analala maana alikuwa halali nyumbani, namshukuru sana Mungu.


KAKA ALIYEKUWA ANAUMWA SASA AMEPONA, NA ALIKUWA NA MADENI SASA ADAIWI TENA
Bwana Yesu asifiwe; Kwa jina naitwa Emalus Justin, ninaishi Kunduchi Mtongani, ni mzaliwa wa Bukoba,   mimi nilikuwa nasumbuliwa na Malaria sana, nimekunywa sana vidonge bila mafanikio, nimeenda katika hospitali nyingi kama Mwananyamala,  nimemeza dawa  sana lakini bado nilikuwa naumwa lakini baada ya kufika mahali hapa na kuombewa sasa nimepona. Na pia nilikuwa na madeni sana, nilikuwa na deni lililofikia 500,000/=, nilikua naogopa sana nikidhania nitafungwa.  Nilikaja kwa Nabii Flora na yeye aliniuliza unadaiwa Shilingi ngapi na mimi nilimtaji kiasi nadaiwa,  Nabii akaniambia nakwenda kufunga hilo pepo la madeni na sasa namshukuru Mungu sidaiwi  tena nimeshamaliza madeni yote.


DADA ALIYEKUWA HAPATI MIMBA SASA AMEZAA MTOTO WA KIKE
Bwana Yesu asifiwe
; mimi nilikuja hapa mwezi wa tisa mwaka jana 2012, nilikuwa na tatizo la kutokupata mtoto, lakini baada ya maombi ya Nabii Flora nikapewa siku 14 nitabeba mimba na kweli nilibeba mimba na sasa nimejifungua mtoto wa kike ndo huyu hapa. Namshukuru sana  Mungu.



KIJANA APONYWA NA KIFAFA, UKILEMA WA MGUU NA MKONO WATOWEKA
Bwana Yesu asifiwe;  Kwa jina ninaitwa Maiko natokea Goba hapa Dar es Salaam, nilikuja siku ya alhamisi wiki iliyopita kwa nabii Flora Peter ili niombewe, nilikuwa na tatizo la kuanguka kifafa, moyo wangu ulikuwa unapanda sana, tatizo linguine nilikuwa na mguu mmoja mfupi  na mkono mmoja mfupi  na mwingine mrefu. Nilikuwa kilema toka kuzaliwa kwangu . Ninamshukuru sana Mungu kwani zamani mwezi ukiisha naanguka kifafa, lakini nilipoombewa sijaanguka tena, namshukuru sana Mungu na Mungu azidi kumlinda mtumishi wake Nabii Flora.
Huyu ni dada aliyeshuhudia huyu kijana akisumbuliwa na kifafa na tatizo lake la ukilema.
MTOTO ALIYEKUWA AMEKUFA MIAKA MI TATU APISHA NA BABA YAKE MAENEO YA TANDIKA YOMBO
Bwana Yesu asifiwe; Kwajina ninaitwa M. Martin Meza, ninaishi Goba jijini Dar es Salaam. Nilifiwa na mwanangu tarehe 12.01.2011, nikamzika Goba. Nikaja kumuona Nabii Flora nah ii baada ya kusikia mafundisho yake. Nikaleta picha hapa kwa Nabii Flora na kuiombea akaniambia mwangu yupo na anapatikana Manzese na saa nyingine  Temeke. Nikaenda Manzese na kuuliza watu wa pale wakanambia ni kweli huyu huwa tunamuona hapa Manzese kuanzia saa 3 usiku na 11 alfajiri. Sikumuona Manzese bali nikaacha tu maagizo, na baadae nikaenda Temeke, na nilipouliza wakazi wa pale Temeke wakasema huwa wanamuona majira ya mchana kuanzisa saa 8 mpaka saa 10, anatoka upande wa mmoja na kwenda upande wa pili na akielekea huko harudi, na akirudi anarudi siku ya pili katika muda huo wa saa 8 na saa 10. Nilihangaika kwa wiki nzima bila ya kumpata, na baadae nikarudi kwa Nabii Flora. Nabii Flora sasa huyu mwanao anapatikana Ubungo, na pia anapatiaka Tandika Yombo. Nikaenda Ubungo na nikazunguka sana, na baadae nikakutana na kijana ambaye sikumfahamu akanisalimia shikamoo baba mara tatu na mimi  nikampita..Baada ya hapo nikaenda Tandika Yombo, nikazunguka kule sana, nikampigia simu Nabii Flora na sikupata bahati ya kuzungumza naye, basi nikarudi na kumfuata Nabii Flora hapa kanisani. Nabii akaniuliza ya kuwa kuna kijana mmoja ulikutana naye na akakusalimia, na alikuwa na nguo Fulani, sasa Yule alikuwa ndiye mtoto wako!  Sasa kutokana na kutomtambua, nimemrudishia jukumu Nabii Flora anisaidie yeye.



DADA ALIYEKUWA KICHAA SASA AMEPONA NA KUMALIZA MASOMO YAKE (MASTERS)
Bwana Yesu asifiwe; Kwa jina ninaitwa Mrs. Kaijage, ninamskukuru sana Mungu kwa sababu tangu nimeombewa na nabii Flora mwaka juzi mpaka leo ninaishi kwa amani. Niliugua sana, niliteseka sana, lakini tangia nilipofiika kwa nabii Flora na kuniwekea mkono. Mimi kipindi cha nyuma nilikuwa nimechanganyikiwa na kuwa kichaa, nilikuwa nikiambiwa niinue mikono juu ili niombewe, ninaanza kuvua nguo zangu . Nabii Flora alinipa siku 21 za kupokea uponyaji wangu, na sasa nimepona. Pia nilikuwa na tatizo la kupata mtoto, nabii Flora aliniombea na kuniambia nitapata mtoto tena wa kiume, na ni kweli nimepata mtoto wa kiume. Mwaka jana 2012 nilimwambia Nabii Flora kuwa ninaenda kusoma Masters, na Ijumaa nimemaliza masomo yangu na kufanya mtihani wangu wa mwisho, na leo ninatoa shukrani yangu kwa kuniwezesha kumaliza masomo yangu salama.
Kushoto ni mwanae aliyempata baada ya kuombewa na Nabii Flora

Mpiga Picha wetu Rumafrica
www.rumaafrica.blogspot.com
Kutoka
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...