Tangazo

Tangazo

NEEMA GASPA KUACHIA ALBAMU MPYA YA NI SHUJAA...

Jumatatu, 4 Agosti 2014

JIUNGE NA CHAMA CHA MUZIKI WA INJILI TANZANIA KWA KUTIMIZA VIGEZO VIFUATAVYO


MASHOGA NA WASAGAJI KUTOKA KENYA NA UGANDA KUFANYA MKUTANO SERENA HOTEL JIJINI DAR

Kama Mtanzania una haki ya kusema na kutoa maono yako juu ya tabia hii ya usagaji na ushoga. Katika vitabu vitakatifu tabi hii imekatazwa na imeonekana ni dhambi kama mwanadamu mwenye akili sawa na asiye na akili sawa anafanya vitendo hivi.

Inasahangaza sana kuona mataifa makubwa na yaliyoelimika na kuwa na maprofesa inaunga mkono vitendo hivi vichafu. Binafsi kutokana na iamani yangu na maadili ya dini yangu ya KIKRISTO ninapiga tabia hii na kama kuna watu wanaunga mkono basi hao ni wao wanahitaji kuombewa ili siku ya mwisho tukamuone Mungu wetu.

Kama Taifa tunawajibika sana katika kuliombea Taifa letu kupingana na hii tabia ya ushoga na usagaji. Hata kama kuna mataifa yanatetea lakini tunatakiwa kusimama na kuwasaidia hawa ndugu zetu wanaoteseka na hili pepo la uzinsi. Inaumiza sana unapoona mwanaume mwenzako anamfanyia mwanaume mwenzake, hii ni aibu sana watu wa Mungu. Umefika wakati wa kufumbua macho yetu na kuwajibika katika kupiana vita na hii tabia isionekane ikitokea nchini kwetu na dunia nzima.

Wenu katika Bwana
Rulea Sanga
RUMAFRICA FOR ALL NATIONS

SOMA HABARI KUTOKA KATIKA MITANDAO MINGINE JUU YA HUU MKASA

MASHOGA kutoka nchi tatu za Afrika Mashariki wamekutana kwa siku mbili jijini Dar es Salaam.

Taarifa zilizopatikana jijini Dar es Salaam, zinasema mashoga hao walikutana juzi katika Ukumbi wa Kivukoni 3 ulioko katika Hoteli ya Serena na kuwashirikisha wasichana wanaofanya mapenzi kinyume na maumbile.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, mashoga hao wapatao 50 walitoka katika nchi za Kenya na Uganda na waliungana na wenzao wa Tanzania.


Katika kuhakikisha malengo ya mkutano huo hayatambuliki, katika ubao wa matangazo wa hoteli hiyo waliutambulisha kama ulikuwa ni mkutano wa kujadili masuala ya kimataifa ya afya ulioitwa International Health (SA).

Mwandishi wetu aliyepata taarifa za uwepo wa mkutano huo, alishuhudia jinsi mkutano huo ulivyokuwa ukiendeshwa kwa usiri wa hali ya juu kwa kuwa kila aliyekuwa akitaka kuingia ukumbini alikuwa akizuiwa.

Pamoja na watu wasiohusika kutotakiwa kuingia ukumbini, hata wahudumu wa hoteli hiyo walikuwa wakiruhusiwa kuingia ukumbini kwa tahadhari ili wasijue kinachoendelea.

Katika kuhakikisha hilo linafanikiwa, mashoga hao walikuwa wakisitisha mjadala kila wahudumu walipokuwa wakiingia ukumbini kwa ajili ya kutoa huduma na mazungumzo yalikuwa yakiendelea baada ya wahudumu kutoka ukumbini.

Pamoja na ulinzi uliokuwa mahali hapo, taarifa zilisema mada kuu iliyowakutanisha mashoga hao ilikuwa ni kujadili changamoto zinazowakabili katika utendaji wao wa kazi. Pia taarifa zinasema walikuwa wakijadili namna ya kufanya utafiti wa kukabiliana na changamoto hizo.

Pamoja na mashoga hao kuonyesha walikuwa wakijadili masuala ya afya ya kimataifa, Msemaji wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Nsachris Mwamwaja, alisema wizara hiyo haikuwa na taarifa za mkutano huo.

Kwa mujibu wa sheria za Tanzania ushoga hauruhusiwi lakini wiki iliyopita Mahakama ya Kikatiba nchini Uganda ilifutilia mbali sheria dhidi ya wapenzi wa jinsia moja, ambayo ilisababisha mataifa kadhaa ya magharibi kuinyima misaada.

Sheria hiyo ilizua mjadala si tu nchini Uganda bali kote duniani kiasi cha kuyafanya mataifa ya magharibi yalazimike kuingilia kati.

Mahakama ilisema muswada uliopitishwa kabla ya kuidhinishwa na rais kuwa sheria, ulipitishwa na wabunge ambao idadi yao haikutosha kuupitisha na kwa hivyo ulikuwa kinyume na sheria.

Sheria hiyo iliharamisha hatua zozote za kueneza au kushawishi mapenzi ya jinsia moja na wakati huo huo ikiwajumuisha wanawake wasagaji katika kundi hilo.

Wabunge nchini Uganda huenda wakalirudisha upya bungeni suala hilo, mchakato unaotarajia kuwa mrefu ukizingatia sheria ya sasa ilichukua miaka minne hadi kupitishwa.

Source: Vituko vya Mtaa
You might also like:

GLORIOUS WORSHIP TEAM WAJA NA NEW LOOK YA COVER LAO LA ALBAMU YA WAWEZA - BADO LIKO JIKONI LINAKARABATIWA

Safari moja huanzisha safari nyingine. Hawa vijana wa Yesu wametoka mbali sana kihuduma. Kazi yao imewagusa walio wengi sana Tanzania na nje ya Tanzania, kinachoshangaza sana ni vijana bado lakini wanafanya mambo makubwa wakishirikiana kama siafu. Inapendeza sana kuona vijana wanafanya kazi ya Mungu. Sio kazi rahisi kwa maisha ya sasa kuona watu wanakaa pamoja na kuacha kazi zao na kuamua kufanya kazi ya pamoja kama hii tunayoona kwa vijana hawa wa GWT



Ukiwakuta hawa vijana wanavyoishi ni kama mtu na dada yake , ni vijana wanaopenda sana kutaniana na pia kufanya kazi kwa pamoja. Mungu wetu na azidi kuwatumia hawa vijana ili wasonge mbele kwa kazi ya Mungu.

Huu ndio muonekano wa kava jipya la albamu ya WAWEZA. Rumafrica katika pitapita mindaoni ilikuta kuna stori kuwa kava hili bado halijakamilika, bado liko jioni linafanyiwa utundu ili lionekane bora zaidi, kwahiyo hata aliyeweza kurirusha mitandaoni amefanya makosa. Tuzidi kusubiri muonekano mzuri wakava hili hapo baadae

KANISA LA UFUFUO LATOA SHUKRANI YA KUPATA HELKOPTA

WAUMINI wa Kanisa la Ufufuo na Uzima linaloongozwa na Mchungaji Josephat Gwajima leo wamefanya ibada ya shukrani kwa kupata helikopta.

Kanisa hilo lililopo maeneo ya Kawe jijini Dar limetoa shukrani zake za dhati kwa Mwenyezi Mungu kuwawezesha kumiliki helikopta hiyo ambayo itatumika zaidi kutoa huduma sehemu mbalimbali za Tanzania na duniani kote.

Helkopta hiyo inakadiriwa kugharimu shilingi bilioni 7.5.

Misa hiyo iliyoanza majira ya asubuhi mpaka jioni ilifanyika kwenye Uwanja wa Tanganyika Packers ambapo ilihudhuriwa na waimba injili maarufu nchini wakiwemo; Rose Mhando, Upendo Nkone, Christina Shusho, Flora Mbasha, John Lissu, Boniface Mwaitege, Munishi na wengineo.


Christina Shusho na Flora Mbasha wakiimba sambamba na waumini wengine waliohudhuria misa hiyo.



Flora Mbasha akiimba katika kanisa la Gwajima.



Halima Mdee akisisitiza jambo alipokuwa akiwahutubia waumini wa kanisa hilo.


Mchungaji Gwajima akicheza kwa shangwe.


Rose Mhando akicheza kwa hisia na shangwe kubwa.


Umati wa watu waliohudhuria misa hiyo wakifuatilia kwa makini.


Upendo Nkone akiimba kwa hisia kali.


Gwajima (kushoto) akicheza pamoja na Christina (Kulia)
.
You might also like:

WAUMINI MORAVIAN KIZIMBANI TENA

KESI inayowakabili waumini 29 wa Kanisa la Moravian lililopo Mwananyamala-Msisiri ” A”, Dar leo imesikilizwa tena Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni chini ya hakimu mwandamizi wa mahakama hiyo, Boniphace Lihamwike.
Waumini hao wanatuhumiwa kufanya fujo hadharani katika Kanisa la Moravian lililopo Mwananyamala-Msisiri ” A” Wilaya ya Kionondoni, Julai 20 mwaka huu na kuzua mzozo uliosababisha waumini kupigana na kusababisha askari polisi kutumia nguvu kutuliza fujo hizo ikiwa ni pamoja na kutumia mabomu ya machozi.
Kesi hiyo imeahirishwa kutokana na baadhi ya watuhumiwa kutokuwepo hadi Septemba 4 mwaka huu itakaposikilkizwa katika mahakama hiyo.

Watuhumiwa wakienda kusomewa mashitaka.

Akina mama ambao ni waumini wa Kanisa la Moravian wakificha sura zao wakati wakitoka mahakamani.

TAMASHA LA UZINDUZI WA ALBAMU YA ROSE MUHANDO YA "PINDO LA YESU " YAFANA DIAMOND JUBILEE DAR


MWANAMUZIKI, Rose Mhando jana amefanya kweli kwa kuwapa mashabiki wa nyimbo za Injili utamu wa Yesu alipozindua albamu ya Pindo la Yesu katika ukumbi wa Diamond Jubilee ambapo mgeni rasmi alikuwa Waziri Mkuu Mstaafu,


Frederick Sumaye na wasanii mbalimbali akiwemo Sarah K kutoka Kenya, Ephraim kutoka Malawi, na wale wa hapa nchini wakiwemo Upendo Nkone, Emmanuel Mbasha, Upendo Kilaeni na wengine.

Katika hafla hiyo Sumaye alitoa ujumbe wa kuitaka Tume ya Uchaguzi ya Taifa na Watanzania kuwa makini ili kuwepo uchaguzi wa haki katika uchaguzi mkuu mwaka kesho.


Rose Mhando akicheka wakati wa uzinduzi wa albamu yake. Nyuma ni waimbaji wake.

Mchungaji Maboya akitoa neno katika uzinduzi huo.

Watu waliofurika katika tukio hilo.

Waziri mkuu mstaafu Fredrick Sumaye (kushoto) akizindua albamu hiyo, pembeni ni Promota wa Muziki wa Injili, Alex Msama.

Mwimbaji Sarah K (kushoto) wa Kenya akiwa na Upendo Nkone.

Emmanuel Mbasha (wa pili kushoto) Upendo Kilaheni pamoja na wadau wengine wakiwa katika pozi.

Waziri mkuu mstaafu Fredrick Sumaye akiwa ameshika album ya ‘Pindo la Yesu’.

Waumini na mashabiki wa Rose Mhando wakipiga makofi.

Sumaye akiwa na Alex Msama (katikati) na Rose Muhando.

Waziri mkuu mstaafu Fredrick Sumaye na mkewe wakifuatilia uzinduzi huo.

Mwandishi wa mtandao huu, Gabriel Ng'osha, na Sarah K.


Jumamosi, 12 Julai 2014

MKURUGENZI WA RUMAFRICA RULEA SANGA AMEFIWA NA SHEMEJI YAKE MBEYA USIKU

Rulea Sanga ambaye ni mkurugenzi wa blogu hii siku ya jana akiwa na masikitiko makubwa sana baada ya kupata taarifa kutoka kwa mtoto wa kaka yake, Furaha Sanga usiku wa kuamkia  jumamosi 12/07/2014 ya kwamba shemeji yake aliyekuwa akimuuguza Muhimbili amefariki dunia.

Rulea Sanga baada ya kupata habari za kifo cha shemeji yake nyumbani kwake Sinza

Mgonjwa huyo ameugua kwa muda mrefu kidogo kwa ugonjwa wa kansa ya mifupa na koo. Ugonjwa huu ulimtesa sana na mpaka ikalazimika kumleta Muhimbili Dar es Salaam. Hali ake ilizidu kuwa mbaya kila kuitwapo leo, na mwisho wa siku madaktari wakaamua kumruhusu aende nyumbani kwani ilionekana ni ngumu sana kumtibu.

Wanafamilia walilzimika kumsafirisha mgonjwa mpaka mkoani Mbeya ambako ni nyumbani wa marehemu. Na leo hii amefariki dunia.

KNOW MORE ABOUT BISHOP JANE K. MUHEGI: FACTORS THAT LED PASTOR JANE MUHEGI INTRODUCE THE DORCUS CHRISTIAN MINISTRIES AND UKUVYU ORGANIZATIONS

Bishop Jane Muhegi. Formerly used to be a teacher. She had a tender heart for the children and youth who no absolute other wise other than to steel and do other immoral conducts which caused the community alert to safe guard themselves from the wrath of such I was blessed to find favor from God and be friend to them.

One day she was bewildered to witness a young man being burnt to death. In spite of her efforts to rescue the boy, she could not help the situation. This moved her spirit and began to find the best ways to help the youth from the destruction.

To manifest God's Love to the disabled, aged, HIV AIDS Victims and widow
Manifest God's love to the misfortune, the needy, the disabled was her objectives number two. We are preaching the word of God and rehabilitating the aged, the homeless and the poor, where we provide them food, clothes and shelter also providing counseling center for AIDS Victims as part of dorcus forums to fight HIV AIDS and its transmission – Bishop Jane!

More about Dorcus Christian Ministries:
P.O. Box 13504 | Tel: +255-22-2650378
Kunduchi Beach - Bahari Beach Road | Dar es Salaam - Tanzania

Healing hour with Bishop Jane Muhegi at Dorcus Christian Ministries

John Shabani giving thanksgiving offering in church at Dorcus Christian Ministries

Dorcus Christian Ministries center



MATUKIO KATIKA PICHA:WINGU JEUSI LATANDA MSIBA WA SISTA ANNA, DAYOSISI YA KUSINI

Msiba wa sista Anna Peterson umeibua simanzi si kwa familia yake tu bali kwa wananchi wa wilaya ya Makete mkoani Njombe alipokuwa akifanya kazi za kijamii tangu ujana wake.

Hayo yamebainika wakati wa ibaada maalum ya kumkumbuka iliyofanyika hii leo katika kanisa la KKKT usharika wa Amani Bulongwa, ibaada iliyoongozwa na baba askofu wa dayosisi ya kusini kati Levis Sanga, Askofu Mstaafu Dkt. Solomon Swallo na Askofu Mstaafu Shadrack Manyiewa pamoja na msaidizi wa askofu Philemon kahuka.


Sista Anna Enzi za uhai wake.

Akihubiri katika ibaada hiyo maalum Askofu Mstaafu Shadrack Manyiewa amesema marehemu alikuwa akifanya kazi zake kwa mkono wa dayosisi ya kusini kati tangu enzi za ujana wake bila ubaguzi ingawa yeye alikuwa mzaliwa wa nchi ya Sweeden.

Amesema amemfahamu toka 1969 na hadi anafikwa na umauti alikuwa akisaidia watoto yatima, wajane, wagane na walemavu wote na hata wasiojiweza na kusisitiza kuwa kanisa haliwezi kumsahau kamwe.

Akielezea historia ya marehemu Askofu mstaafu Dkt Solomon Swallo amesema Sista Anna alikuwa akifanya kazi zake kwa kujituma bila kujali ugumu wa kazi uliokuwepo kwa kipindi hicho hasa ubovu wa barabara na ugumu wa kuwafikia wananchi kutokana na tabu ya usafiri.

Askofu mstaafu Manyiewa akihubiri ibadani hapo.

Dkt Swallo amesema alikuwa akisisitiza kuwa Mungu ndiye aliyemtuma kufanya kazi Bulongwa Makete na si Binadamu hivyo haoni shida kutumikia jamii ya Makete toka ujana hadi uzee wake.

Askofu mstaafu Dkt Solomon Swallo.


Dkt Nicodemas Kikoti.

Kwa upande wake Kaimu Mganga mkuu hospitali ya Bulongwa Dkt Nicodemas Kikoti amesema marehemu pia alikuwa akifanya kazi na hospitali hiyo pamoja na jamii ikiwemo kusomesha watoto yatima kutoka shule ya awali mpaka vyuo, kuwajengea nyumba wasiojiweza, kuhudumia wajane, kusaidia vifaa vya umeme pamoja na kujenga makao ya kituo cha watoto yatima Bulongwa.


Mch. Dkt Phares Ilomo.

Naye Mch. Dkt Phares Ilomo kutoka chuo Kikuu cha Iringa amesema yupo tayari kuandika kitabu cha kuelezea historia ya marehemu Sista Anna kwa kushirikiana na viongozi wengine wa kanisa na washarika kuchangia gharama ili kitabu hicho kichapishwe na kuzalishwa kwa faida ya vizazi vijavyo ikiwemo kukiweka katika maktaba ya chuo chake.

Waziri wa nchi ofisi ya makamu wa rais mazingira Dkt Binilith Mahenge ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Makete akitoa salamu za rambirambi amesema marehemu alikuwa akifanya shughuli ambazo kimsingi zilitakiwa kufanywa na serikali hivyo wema wake kwa jamii ya Makete hauna mfano.


Waziri wa nchi ofisi ya makamu wa rais mazingira Dkt Binilith Mahenge ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Makete akitoa salamu za rambirambi.

Amesema njia pekee ya kumuenzi ni kufanya yale aliyoyapenda huku akisisitiza kuwa serikali itashirikiana na kanisa kuendeleza kazi zote alizoziacha Sista Anna.


Askofu wa dayosisi ya kusiki kati Levis Sanga.

Askofu wa dayosisi ya kusiki kati Levis Sanga ametangaza tarehe 26 Juni kila mwaka kuwa ni siku maalum kikanisa ya kumkumbuka marehemu sista Anna hivyo jamii inashauriwa kufika kwenye kituo cha watoto yatima Bulongwa kwa ajili ya kuwatembelea na siku hiyo itakuwa ikifanyika ibaada maalum kwa ajili ya marehemu.

Sista Anna Peterson amefariki Juni 26 mwaka huu nchini Sweeden alipokwenda kwa ajili ya matibabu na amezikwa leo hii nchini humo, na hapa Makete alikokuwa akiishi toka ujana wake imefanyika ibaada maalumu ya kumkumbuka.

Mungu ailaze mahali pema peponi roho ya marehemu Sista Anna Peterson, Amen.

Habari/Picha Na Edwin Moshi, Makete

JAMANI TUMUOMBEE NDUGU YETU ORIDA NJOLE

Kwa wale wasiomjua Oride Njole, ni mwimbaji wa nyimbo za Injili Tanzania. Leo hii yuko kitandani anaumwa, anatamani kuwa kama wewe ambaye kwa sasa unacheka na kufurahi lakini anashindwa kutokana na ugonjwa alionao. Jamani ndugu yetu anaumwa sana tunapaswa kumuombea na ikiwezekana tufike pale hospitalini Temeke hospitali ya serikali.


Orida Njole

RUMAFRICA YAPATA TAARIFA ZA UGONJWA

Rumafrica imepokea habari hizi siku ya leo kwa njia ya simu kutoka kwa mtangazaji wa Radio Tumaini Obedi Kikao, anasema hali yake sio nzuri sana, ndugu yetu anateseka sana. Kama binadamu mwenye huruma basi fika pale hospitalini kumpa pole ndugu yetu huyu. Kumbuka ulikuwa naye kipindi mnacheka leo hii mwenzetu amenuna kutoka na maumivu anayopata. Anahitaji faraja kutoka kwako Mtanzania.



NDUGU NA MARAIKI
Kumbuka wewe rafiki uliyekuwa unacheza naye mpira wa mikono, Oride ni mwanamichezo mkubwa sana na amekuwa nawe katika michezo mbalimbali, lakini leo hii anashindwa hata kushika mpira kutoka na ugonjwa alionao. Umefika wakati wa kwenda kumuona ndugu yetu na kubwa zaidi ni maombezi.


WACHUNGAJI NA WATUMISHI WA MUNGU

Mchungaji ambaye ulikuwa ukimtumia Oride Njole katika huduma yako, ameimba sana kanisani kwako lakini leo hawezi kuimba tena kutoka na kile kinachomsumbua. Nenda basi ukamuombee pale kitandani alipolala ili aweze kuamka na kufanya kazi ya Mungu kama zamani. Kuwa na moyo wa huruma basi.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiOwQlqihwXMe7mtHGAYjwMIxXNXaKa3ylVTXlyMU_b064YZ6CWsOBNnL_JVRk_qhCTxE4YZseoSeqx9QRhaoiM3P0Q0O9fXbtnJ3PF0kgGrqhmsEv0AoUndF4TymZQ0A6YRVDlhgMNjII/s640/orida6.jpg
Orida Njole akimtumika Mungu kanisani

Hata wewe mchungaji ambaye unayemfajhamu na wewe uliyemfahamu kwa kupitia blogu hii ya Rumafrica basi acha hicho unachofanya sasa anza kumuombea. Ondoa hiyo roho inayokusukuma usimmuombee na ikemee sasa.

WANAMICHEZO
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgtSKeClRxnGGLHMRIm0KLRhFAsa3O1rWw2qG4fc7DNTbseXoRJJudINkaER5Gp-vxrYKiFrIUgG_VXWstq6aOSgmdCxUys2XP7ajybraUCcvGSq2_5DSx9XPmkm-iUj6TD8i4YsyABHbo/s640/DSCN7837.JPG
Orida Njole (kushoto)

Marafiki zake ambao mmekuwa naye studi kurekodi nyimbo za kumtukuza Mungu, sasa tunawaomba mfanye maombi na kufika pale hospitalini kumtia moyo na kumpa pole. Mmekuwa mkicheka na kupeana mawazo studio lakini leo hii mwenzenu anashindwa hata kuwapa mawazo kutokana na maumivu anayopata. Kuwa na moyo wa upendo na huruma kama vile mnavyotuimbia sisi tuyafanye yale manyoimba.
http://photos-a.ak.fbcdn.net/hphotos-ak-ash3/t1.0-0/c0.2.960.639/s720x720/379618_192151074260838_1925803444_n.jpg
Orida Njole kushoto wa kwanza
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjW-n0ja52JJmz4DHQzOMdonN3qU6qULdyiNcyhieky96DWpV2mAPzeokGULBpJSFNYTJN_ypZ7rwcvNWNqlqm8fLA2pvo-mIf57eTRjb9ahug9RpmGTATPQL06l3v-5lRtLP89n8XPFox3/s640/Orida-Njole-Poster.jpg
DVD Cover la albamu ya Orida Njole

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEihY5UGc2CuKXDwnICXieiqP7SFgrIPC0qKrsQn9yPzSl7Ohu8v4PKy-xS3-C18TLftqdmJoxhlin-hdlMiX624nluK3nZbNxOPsgdZSNNHMjuOC3B2wtNTdBQe2g8ry_PsRJl7WXLMfBpc/s640/Orida.jpg
Orida Njole
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...