Tangazo

Tangazo

NEEMA GASPA KUACHIA ALBAMU MPYA YA NI SHUJAA...

Jumatatu, 4 Agosti 2014

TAMASHA LA UZINDUZI WA ALBAMU YA ROSE MUHANDO YA "PINDO LA YESU " YAFANA DIAMOND JUBILEE DAR


MWANAMUZIKI, Rose Mhando jana amefanya kweli kwa kuwapa mashabiki wa nyimbo za Injili utamu wa Yesu alipozindua albamu ya Pindo la Yesu katika ukumbi wa Diamond Jubilee ambapo mgeni rasmi alikuwa Waziri Mkuu Mstaafu,


Frederick Sumaye na wasanii mbalimbali akiwemo Sarah K kutoka Kenya, Ephraim kutoka Malawi, na wale wa hapa nchini wakiwemo Upendo Nkone, Emmanuel Mbasha, Upendo Kilaeni na wengine.

Katika hafla hiyo Sumaye alitoa ujumbe wa kuitaka Tume ya Uchaguzi ya Taifa na Watanzania kuwa makini ili kuwepo uchaguzi wa haki katika uchaguzi mkuu mwaka kesho.


Rose Mhando akicheka wakati wa uzinduzi wa albamu yake. Nyuma ni waimbaji wake.

Mchungaji Maboya akitoa neno katika uzinduzi huo.

Watu waliofurika katika tukio hilo.

Waziri mkuu mstaafu Fredrick Sumaye (kushoto) akizindua albamu hiyo, pembeni ni Promota wa Muziki wa Injili, Alex Msama.

Mwimbaji Sarah K (kushoto) wa Kenya akiwa na Upendo Nkone.

Emmanuel Mbasha (wa pili kushoto) Upendo Kilaheni pamoja na wadau wengine wakiwa katika pozi.

Waziri mkuu mstaafu Fredrick Sumaye akiwa ameshika album ya ‘Pindo la Yesu’.

Waumini na mashabiki wa Rose Mhando wakipiga makofi.

Sumaye akiwa na Alex Msama (katikati) na Rose Muhando.

Waziri mkuu mstaafu Fredrick Sumaye na mkewe wakifuatilia uzinduzi huo.

Mwandishi wa mtandao huu, Gabriel Ng'osha, na Sarah K.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...