Tangazo

Tangazo

NEEMA GASPA KUACHIA ALBAMU MPYA YA NI SHUJAA...

Jumatatu, 10 Februari 2014

MATENDO MAKUU ANAFANYA MUNGU KATIKA KANISA LA YESU KRISTO HUDUMA YA MAOMBEZI NA UPONYAJI KWA NABII FLORA

Watu wazidi kushuhudia yale Mungu anafanya katika maisha yao, baada ya kufanyiwa maombi na mtumishi wa Mungu Nabii Flora. Watu wamekuwa wakitumia sticker na sabuni zilizoombewana Mtumishi wa Mungu na wengine wakipokea miujiza yao kwa maombi tu. Hakika Mungu hujibu kwa maana haya tunayaona na kuyasikia kwa waliotendewa. Ni muda wako sasa wa kufanyiwa jambo na Mungu, unatakiwa kuwa mnyeyekevu na kufuata taratibu za Mungu. Tusome baadhi ya shuhuda.

SHUHUDA ZA JUMAPILI 02.02.2014

DAUD UKUSEMAKUSEMA ANAMSHUKURU MUNGU BAADA YA KUOGEA SABUNI ILIYOOMBEWA NA NABII FLORA, KATIKA KAMPUNI ANAYOFANYA KAZI AMEWEZA KUPATA MKOPO WA KUMWEZESHA KUFANYA BIASHARA ZAKE

Bwana Yesu asifiwe, naitwa Daud Ukusema; natoa shuhuda kutokana na sabuni hizi alizotupa Nabii Flora, nilitumia hii sabuni nikaiogea, sasa wiki hiyo hiyo nikawa nimeandikiwa barua, kwamba niandike mchanganuo wa biashara, kwamba mimi naweza nikafungua biashara nikafanya kwaajili ya mahitaji yangu mimi. Biashara ile niliandika mchanganuo mzuri sana kwa sababu nimepitia biashara nyingi, baada ya kuandika mtaji ulikuwa ni mkubwa sana lakini bosi aliniambia mtaji sio shida, kwa hiyo wiki hii nitakupa. Pia akaniambia niwaandikie na wengine watu watatu kwenye kampuni yetu ili tuweze kuwakopesha, alafu watakuwa wanarudisha kidogo kidogo. Ni miaka mingi niliangaika, lakini kwenye hiyo kampuni nimewatumikia kwa muda wa miaka miwili sasa, na ndio wanataka kunipa huo mkopo, namshukuru sana Mungu.


SHUHUDA YA JUMAPILI 02.02.2014

DIANA SAMWELI ANAMSHUKURU MUNGU MAMA MKWE WAKE ALIYEKUWA ANAPUMULIA OXYGEN MUHIMBILI SASA ANA NAFUU, PIA BINTI YAKE ALIYEANGUKA NA KUZIMIA SASA ANAENDELEA VIZURI

Bwana Yesu asifiwe, naitwa Diana Samweli; kwanza napenda nimshukuru Mungu wa Nabii Flora, maana anafanya anatenda na kuzidi, mama mkwe wangu alikuwa anaumwa, Ijumaa ilikuwa nije maana nakujaga ibada ya jioni, nilijipanga lakini nilishindwa. Mama mkwe wangu alikuwa anaumwa akapelekwa Mwananyamala, baada ya kupelekwa mwananyamala, nikaambiwa amelazwa BP ipo mpaka 40. Nikasema itarudi ilipotoka haiwezekani, baada ya muda nikajipanga nikasema naenda Mwananyamala, nikaambiwa anapelekwa Muhimbili. Nikasema imekuwaje, wakasema amekuwa hali sio nzuri sana amewekea na oxygen, mimi nikaoga nikawaambia watumishi sitakuja kwenye ibada, wakati natoka barabarani shemeji zangu wakanipigia simu wakaniambia inakuwaje, nikawaambia Mungu wa Nabii Flora, tunayemwabudu, wa Kanisa la Maombi na Uponyaji Salasala, Mungu aliyehai atatenda miujiza. Basi kabla sijapanda gari nilichukuwa mkono wangu nikapuliza pumzi ya uzima, nikasema pokea uponyaji, baada ya muda operation ile aliyokuwa amefungwa na ile oxygen aliyokuwa amewekewa akaanza kuwa vizuri. Baada ya muda tukaelekea Muhimbili, mapaka saa nne usiku tulikuwa mapokezi, nikasema shetani umepangiwa plate namba hapa tumeshaingia, tulipofika hodini Daktari akasema huyu mgonjwa tunatakiwa tumcheki vipimo vyote, nikamwambia Doktari huyu mgonjwa amekwisha kupona oxygeni inaondolewa. Akasema hii ni machine imewekwa na Daktari, nikasema nani bingwa kama Mungu, akasema basi Mungu wako na afanye, walipomwingiza kwenye vipimo oxygen ikatolewa. Pili jana jirani yangu alikuwa na sherehe akataka niende, nikamwambia sitaweza kuja mimi nakwenda Hospitalini, wakati nipo njiani nikapigiwa simu mtoto wangu ambaye anaitwa Beatrice tunasali naye hapa amedondoka, amezimia ameng’ata ulimi. Nikamwambia shetani usini beep mimi nakupigia, nikaanza kupambana na yale malango ya kuzimu, shetani akaachilia kwa jina la Yesu. Wakati wanampeleka IMTU baba akanipigia akaniambia upo wapi, nikamwambia nipo njiani nakuja, wakati natafuta gari Roho wa Bwana akaniambia ingia magotini. Mimi nikaingia magotini kwa ujasiri nikamwambia Mungu wa Nabii Flora, ulisema tutaona wazi wazi, nataka sasa nione wazi wazi, namshukuru Mungu hali ya mgonjwa Muhimbili inaendelea vizuri, na pia hali ya binti yangu inaendelea vizuri.
DIAMOND MATHIAS ANAMSHUKURU MUNGU KWA KUMPONYA GANZI MWILINI
Bwana Yesu asifiwe, naitwa Dimond Mathias; naishi Salasala Kilimahewa, Nabii Flora amenitendea mambo makubwa sana, mwili wangu ulikufa ganzi ukawa haufanyi kazi. Nikaja hapa nikamwelezea Nabii, Nabii akaniambia chukuwa Zabibu, basi akaniombea ile zabibu akaniambia utakwenda kuogea kwa muda wa siku tatu. Siku ile ile nikaona mwili unafanya kazi vizuri, namshukuru sana Mungu wa Nabii Flora anaponya.


 FINA ANAMSHUKURU MUNGU BAADA YA KUJA KWA NABII FLORA NA KUOMBEWA AMEWEZA KUKABIDHIWA FREMU YA CHAKULA NA BIASHARA INAKWENDA VIZURI

Bwana Yesu asifiwe, naitwa Phina; namshukuru Mungu wa Nabii Flora, nilikuja hapa siku ya Jumanne, nilikuwa nimekabidhiwa fremu ya chakula na kila kitu. Wakati nakuja hapa ilikuwa muda wa jioni, nilikuwa nikimpigia huyo baba simu kuanzia asubuhi mpaka jioni hapokei simu. Nilivyoonana na Nabii Flora nikamwelezea, nikatoka hapa kufika hapo nje nikampigia Yule baba simu, akapokea simu yangu akaniambia tukutane pale kwenye ile fremu. Nikakutana naye pale akanikabidhi fremu na kila kinachuhusu chakula, baada ya hapo nikachukuwa ile funguo nifanye usafi ili kesho yake nianze biashara, wakati nafanya usafi kuna vitu vilikuwa vimewekwa kule ndani kutoka kwa waganga. Kulikuwa na kitambaa cheupe kimezungushwa na uzi mweusi, jioni nikafunga fremu, asubuhi yake nikaanza kupika. Kupika pale biashara haikwenda chapati zikabaki zote, chai ikabaki, supu haikuchukuliwa wala maharage, nikaja hapa tena kwa Nabii jioni nikamwelezea, baada ya kumwelezea akaniambia vitatoka vitu vyote na biashara itaisha. Nilitoka hapa saa kumi na mbili nikafika pale kwenye fremu yangu, watu wakanishauri pika sasa hivi kuna wateja, nikawaambia sasa hivi muda umeenda, lakini mume wangu aliniambia umetoka kwa Nabii pika. Nikapika chakula mchele kilo nne, zile chapati za asubuhi zikaisha muda ule, namshukuru Mungu mpaka sasa hivi biashara inaendelea vizuri, na vile vitu kutoka kwa waganga vimetolewa. Na Yule baba amekuja jana kunikabidhi fremu iwe mali yangu, namsahukuru sana Mungu wa mahali hapa.

 GRACE ANAMSHUKURU MUNGU BAADA YA KUTUMIA SABUNI ILIYOOMBEWA NA NABII FLORA AMEPATA KAZI

Bwana Yesu asifiwe, naitwa Grace; Jumapili iliyopita nilichukuwa sabuni nikaenda kuogea, namshukuru Mungu amenifungua nimepata kazi. Nimekaa kwa muda wa miaka 4 sijapata kazi, lakini baada ya kutumia hii sabuni nimepata kazi, na nimeaanza Jumanne iliyopita.


 GRACE JOHN ANAMSHUKURU MUNGU KWA KUPATA MUUJIZA WA FEDHA

Bwana Yesu asifiwe, naitwa Grace John natokea Goba; Namshukuru Mungu wa Nabii Flora amenipa pesa, shilingi elifu hamsini na tatu, namshukuru sana Mungu

 KOLETO SAMBANO ANAMSHUKURU MUNGU BAADA YA KUOGEA SABUNI ILIYOOMBEWA NA NABII FLORA AMEPATA KAZI

Bwana Yesu asifiwe, naitwa Koleta Sambano; namshukuru Mungu baada ya kuogea ile sabuni nimepata kazi, na nimeaza jana, namshukuru sana Mungu wa Nabii Flora.


 MAIMUNA ANAMSHUKURU MUNGU WA NABII FLORA KWA KUMPONYA VIUPELE MWILINI BAADA YA KUOGEA SABUNI ILIYOOMBEWA NA NABII, PIA MUME WAKE AMEPATA KAZI BAADA YA KUTUMIA SABUNI ILIYOOMBEWA NA NABII FLORA

Bwana Yesu asifiwe, naita Maimuna; nilikuja mahali hapa nikiwa naumwa, nilikuwa na vipele, nilionana na mtumishi Nabii Flora, nikamwambia naumwa nimetokwa na vipele mwili mzima. Akaniambia utaponywa, utachukuwa sabuni ukifika utaogea na utapona, kweli namshukuru Mungu nimepona. Alafu kupitia sabuni hiyo hiyo mume wangu alikuwa hana kazi kwa muda wa miaka 2, aliomba kazi sehemu akaenda kufanya interview akawa ameanguka. Lakini nilivyoipata hii sabuni ile wiki ya kwanza Nabii alivyogawa, baada ya kuitumia hii sabuni, akapigiwa simu akaitwa kazini akaambiwa akaanze kazi. Nikamwambia Nabii Flora japo amepata kazi lakini nataka wale aliowakuta pale kazini awafunike yeye awe juu, na kweli wapendwa ndivyo ilivyokuwa, alipofika pale kazini amewekwa officer mwajiri, namshukuru sana Mungu.

 MAMA ANAMSHUKURU MUNGU WATOTO WAKE WAMESHINDA KESI PIA WAMEPATA WACHUMBA BAADA YA KUTUMIA STICKER, SABUNI NA KUOGEA MAJI YALIYOOMBEWA NA NABII FLORA

Bwana Yesu asifiwe; siku moja nikiwa kazini jirani yangu aligombana na mabinti zangu, ilikuwa ni kwa sababu ya kamba, yeye aliikata ile kamba ikaanguka chini, mwanangu akaja akamwambia, sasa wakawa wameshikana. Yule jirani akaondoka akaenda polisi, mimi nilikuwa sina habari akawaweka ndani, mida ya saa moja nikapigiwa simu wanao wapo rumande. Nikachukuwa sticker yangu nikaiweka kwenye kifua, nikasema kupitia Nabii Flora nitapiga goti sana, nikachukuwa ile sticker nikaiweka kweye kifua. Nilipofika tu pale mkuu wa kituo akaniambia mama wewe ndio mwenye watoto, nikamwambia ndio, akaniambia mimi nimeona watoto wako hawana hata kesi kubwa watoe tu, namshukuru Mungu saa nne nikawatoa watoto wangu. Niliambiwa ni tarudi siku nyingine kwaajili ya kesi, basi siku hiyo nikaja hapa, kuonana na Nabii Flora, namshukuru sana Nabii siku hiyo alitatisha ibada akanisikiliza shida yangu, Nabii akaniombea akaniambia naifunga hiyo kesi. Kweli asubuhi yake nikaenda kule, na wale mabinti walikuwa na sabuni, , wakaogea zile sabuni na mwingine ambaye alikuwa haji kusali hapa nikampa maji akaogea, tulipoingia pale polisi wakasema naona hawa mabinti hawajanywa cha, nikamwambia kweli naona wana hofu sana, akawaambia basi chukuweni hii elfu mbili mkanywe chai. Tuliporuddi tena tukamkuta Yule mama ambaye ni jirani yetu, akapiga magoti akasema sijaongea lolote naombeni mnisamehe. Mimi napenda kusema Watanzani na waumini wenzangu, Nabii Flora anaweza amenisaidia katika mambo mengi sana. Na watoto wangu wote wawili wamepata wachumba, kwa kweli namshukuru sana Mungu wa mahali hapa.

PENDO SAID ANAMSHUKURU MUNGU BAADA YA KUOMBEWA NA NABII FLORA BABA WATOTO WAKE ALIKUWA AMPI PESA YA MATUMIZI LAINI SASA ANAMPA, PIA AMEPONYWA VIDONDA VYA TUMBO

Bwana Yesu asifiwe, naitwa Pendo Said; nilikuja kwa Nabii Flora nikamwambia toka mwaka 2006 baba watoto wangu ananidharau, nikienda kwake ananifukuza, nikimuomba pesa ya matumizi ananinyima. Jumapili wakati Nabii anaomba alisema tushikanishe mikono, nikafanya hivyo, alafu akasema uwe unamwita huyo mume wako au mpenzi wako, basi mimi nikawa namtaja. Baada ya ibada kuisha, nikakuta amenitumia meseji, akasema kesho nitakutumia pesa ya matumizi, pamoja na pesa ya kodi, Jumatatu akawa ametuma. Pia namshukuru Mchungaji July nilikuwa naumwa na vidonda vya tumbo, akaniambia nizunguke hapa Kanisani mara saba, huku nikisema Mungu asante, toka siku hiyo nimepona kabisa vidonda vya tumbo, namshukuru sana Mungu wa Nabi Flora.

RICHARD MGOGO ANAMSHUKURU MUNGU KWA KUMPONYA, PIA AMEITWA KAZINI

Bwana Yesu asifiwe, naitwa Richard Mgogo; juzi nilikuja kwa Nabii hapa kuna watumishi walikwazika, nilikuwanakimbilia kwa mtumishi ili nipone, Alhamisi ya juzi nilikuwa ninaumwa mwili mzima, nusu ya kufa. Nikamtafuta dada yangu Lugano kwenye simu akawa hapatikani, namba ya Nabii nilikuwa sina, kuna dada mmoja anaitwa stella akaniambia hiyo ni roho ya mauti kwa hiyo kemea, niliingia kwa imani ikakemea. Taratibu nikaanza kupona, nikaja hapa nikamkuta mtumishi amekaa, nikamfuta nikamwelezea. Pia nilikuwa nimeitwa kwenye ajira, nikamwambia nimekuja kwa sababu nilikwa naumwa nimepona, naomba unipe ulinzi tamka neno lolote. Pia kuna ajira nilikuwa nimeitiwa, nikaenda kufanya interview, wakaniambia kazi yangu ipo ya offcer muajiri, kabla sijaja hapa walikuwa wananisumbua sumbua. Sasa baana ya maombi ya hapa nikapigiwa simu, kumbe ni mganga wa kienyeji alikuwa ananisumbua. Huyo mganga nilikuwa naumwa tumbo nikiwa Mbeya, akaniambia wewe unaumwa tumbo mimi ninadawa, basi akaenda kuniletea dawa ya asili nikanywa, kumbe alikuwa ananichezea kachukuwa nyota yangu. Nilisimama mpaka sasa hivi namshukuru Mungu nipo salama, ila taabu anayoipata huyo mganga Mungu anajua. 

STELLA PHILEMON ANAMSHUKURU MUNGU BAADA YA KUTUMIA STICKER ILIYOOMBEWA NA NABII FLORA AMEWEZA KUJIWA BARUA YAKE YA KUOMBA MKOPO NA AMEPATA PESA ALIZOKUWA ANAHITAJI

Bwana Yesu asifiwe, naitwa Stella Philemon; ninamshukuru Mungu kupitia madhabahu hii ya muheshimiwa Nabii Flora, Mungu ameweza kutenda yale ambayo ni kinyume na utaratibu kupitia sticker. Jumapili iliyopita nilichukuwa sticker mahali hapa, kazini kwangu tulipata barua kwamba tunatakiwa kwenda Nairobi kwaajili ya Training. Mwaka uliopita tulikwenda Nairobi kwaajili ya training na tulikaa kule kwa muda wa miezi miwili, na baada ya kukaa hiyo miezi miwili tuliambiwa tutarudi tena mwezi mmoja, kwa kawaida hiyo training itakuwaga ya miezi 3. Basi kulingana na taarifa hizo, nilikuwa na mashaka kulingana na kwamba ninatakiwa kulipa ada ya mtoto wangu anayesoma chuo cha ardhi hapa Dar es salaam. Niliandika barua ya maombi na kulinga na ada ile natakiwa kulipa milioni moja na laki nne, ilinibidi niombe mkopo kazini wa milioni moja kwanza, ili nikienda Nairobi mwezi wa pili binti yangu anayefungua shuke mwezi wa tatu aweze kuendelea na masomo. Basi baada ya kuandika ile barua, nikaipeleka officen kupitia mkuu wa kituo, niliambiwa kwamba hiki ni kinyume cha utaratibu, huwezi kukopa pesa nyingi kiasi hiki, inatakiwa pesa utakayolipa iwe ndani ya miezi 3 uwe umesharudisha. Ile baraua ilivyopitiwa ikaonekana kwamba haiwezekani mapaka nimuone National director, niliingia ndani ya chumba cha maombi nikimsubiri National director kuongea naye, wakati niimsubiria alikuja officer mwajiri, akaniuliza unashida gani, nikamwonyesha ile barua nikamwambia kwamba ninashida ya ada, na ada inayotakiwa ni milioni moja. Basi Yule officer mwajiri akaniambia kwamba hicho ni kitu ambacho hakiwezekani, na hauwezi kwenda kwa National director mpaka upitie kwangu mimi na kwa National accountant. Nilikwenda chumbani nikachukuwa sticker yangu nikaishika mkononi wakati nikiongea na National director, na moja kwa moja ile barua ilisainiwa na nikapata mkopo, namshukuru sana Mungu wa mahali hapa.

VERONICA ANAMSHUKURU MUNGU WA NABII FLORA KWA KUWEZA KUTAMBUA KIFO CHA MTOTO WAKE KIMETOKANA NA NINI

Bwana Yesu asifwe, naitwa Veronika; Alhamisi nilipigiwa simu kwamba mwanangu anaumwa, alikuwa na hali mbaya, sasa wakati natafakari Ijumaa nikapigiwa simu kwamba mwanangu kafariki, mtoto wangu alikuwa kwa baba yake anaishi Temeke. Wakati nafakari kwa nini amekufa, sasa wakati sijapata jibu nikamwelezea rafiki yangu Teresia, akaniambia twende kwa Nabii, lakini kila nikitaka kushukuru Roho yangu inakuwa nzito, nikamwambia Teresia ngoja kwanza niende kwa Nabii, ili nijue moja wapo kama kweli mwanangu kafa katika kifo cha Mungu au la. Kweli nikaja nikaomba kibali nikawakuta watumishi wa Mungu wakaniruhusu, nikaonana na Nabii, akaniambia mwanao ajafa amechukuliwa msukule. Ila cha kufanya ukienda usilie na wala usiongee chochote, lakini kuna vitu ambavyo utakuwa unaviona, ni kweli nikaenda pale, lakini kabla sijaondoka hapa Nabii alinipa sticker akaniambia niiweke ndani ya nguo. Kufika pale nikamshukuru Mungu nikawa nasali, nikasikia Roho Mtakatifu ananiambia, zunguka nyumba na kuharibu uchawi iliopo ndani ya nyumba hii, kweli nikanyanyuka nikazunguka, ndugu zangu wakawa hawaamini walisema nikitoka hapa nitaenda kufanya fujo. Nikawaambia hapana siwezi kufanya fujo nimetoka kwa mtumishi wa Mungu Nabii Flora, baada ya hapo nilishangaa sana, baba yake alikuwa aniangalii usoni wala kunitazama. Tulipozika tukamaliza Yule baba alikimbilia kituo cha polisi, akaenda kusema mimi ndio niliyemuua mtoto wangu kwa nguvu za giza, kwa kweli Mungu wa Nabii Flora anatenda kazi.

 VUMI RAMSON BENJAMINI ANAMSHUKURU MUNGU KWA KUMPONYA UVIMBE KWENYE MAZIWA

Bwana Yesu asifiwe, naitwa Vumi Ramson Benjamin; namshukuru Mungu wa Nabii Flora ameniponya ziwa, kwa maana niliangaika kwa muda mrefu, nilienda Temeke Madaktari wakashindwa kwa sababu ziwa lilikuwa na uvimbe. Nilipotoka hapo wakaniambia niende Ocean Road, nilipofika pale ilikuwa muda wa saa nane, niliyemkuta pale akaniambia dada umekuja umechelewa kwa hiyo siwezi kukupa hii kadi ya kuonana na Daktari, mpaka tusaidiane na mimi nikusaidie. Nikasema Mungu wangu haitaji rushwa mimi nitaonana na Daktari na atanisaidia, baada ya dakika chache nikashangaa Yule Daktari kafika pale, akataka kuchukuwa form za wagonjwa, akakuta form hazijajazwa. Akauliza kuna watu hapa wanataka kuchekiwa maziwa, tukasema tupo tulikuwa watu watatu, basi akatuchukuwa akatupandisha na lifti mpaka ghorofa la tatu. Katika kuchekiwa mimi nilikuwa mtu wa pili, wenzangu walichekiwa wakakutwa na viuvimbe vidogo vidogo, lakini walichajiwa pesa nyingi kutoa vile viuvimbe ili vikapimwe Muhimbili wajulikane kama wana saratani au hawana. Lakini mimi nikiwa pale nilikuwa namuomba sana Mungu wa Nabii Flora, nikasema naomba kwa sababu uvimbe wangu ulikuwa ni mkubwa, nikaomba nisikutwe na saratani nipewe vidonge tu. Basi Yule Daktari kuniangalia akasema dada ziwa lako linatisha ngoja nimpigie Daktari mbingwa simu aje akucheki. Kweli akaja huyo Daktari bingwa akaniangalia akashangaa, akaniuliza dada unatatizo gani, basi nikamwelezea kote nilipokwenda. Akaniambia sasa sikiliza, nitakuandikia dawa ukatumie kwa muda wa siku kumi, kama uvimbe utaendelea kuwepo utakuja ili tujue tatizo ni nini. Nilichukuwa dawa juzi nikatumia jana tu, leo naona uvimbe wote umeisha, namshukuru sana Mungu wa Nabii Flora, Mungu wa Nabii Flora kweli anaweza na anaponya, ukimtegemea utaishi kwa amani.

SHUHUDA ZA TAR 4.FEB.2014

DUSTAN AMSHUKURU MUNGU BAADA YA KUOMBEWA NA NABII FLORA AMEWEZA KUPONA MAPEPO NA AMEPATA KAZI NA AMEWEZA KUNUNUA KIWANJA
Bwana Yesu asifiwe, naitwa Dustan Ezekiel; Bwana amenitendea makuu katika madhabahu hii, nilikuja hapa nikiwa naumwa sana, kila siku nikija hapa lazima nianguke mapepo, ni miaka mingi naugua mapepo. Nilikuwa kila ninachokishika sifanikiwi, nilipofika hapa mwaka jana mezi wa 11 Nabii akaniambia hutatoa pesa tena kununua kazi, Nabii akaniambia nihudhurie maombi kwa siku 21. Niliudhurika kama siku tatu Nabii akiniombea, nikapata kazi kwa wachina, nikafanya kazi kwa muda mdogo tu nikafanikiwa, nilipopata pesa nikanunua kiwanja. Baada ya hapo kwa wachina pale nikapumzishwa, basi nikawa nakuja tu huku kwa Nabii, baada ya muda nikaona tena Mungu amefungua milango yangu, niliitiwa kazi ya serikali ya kuandika taarifa za bima, wakati nasubia ile nikaitiwa tena kazi nyingine ya barabarani. Siku ya kwanza nilipokuja hapa nilikuwa nimevalishwa mavitambaa, nikasema kwasababu nimeshafika kwa Mungu basi nikayatupa yale mavitambaa, namshukuru Mungu baada ya kufika hapa nimefanikiwa mambo mengi sana.

DADA BAADA YA KUTUMIA STICKER YA NABII FLORA KAZI ZAKE ZINAKWENDA VIZURI PIA ANAOWADAI WANAMLIPA
Bwana Yesu asifiwe; mimi nilikuja hapa siku ya Jumapili, ni mwimbaji siku hiyo sikuimba lakini nilipata muujiza mkubwa zaidi ya kuimba. Nilichukuwa hii sticker ya Nabii Flora, mimi huwa nafanya Secretarial services Tegeta, nilipofika pale, nikaomba nikasema kwa jina la Yesu najiambatanisha na Mungu wa Nabii Flora, leo nikaone tofauti. Cha ajabu alikuja mzee mmoja akaniletea kazi yaku duplicate DVD ya Mwislamu (kaswida). Baada ya hapo akawatuma vijana wakaja kuchukuwa ile kazi akalipa nusu, nikawa namdai laki moja na usu, cha kwanza nilipofungua pale nikamuona Yule baba anakuja haraka haraka. Akaniambia dada nilikuwa na mambo mengi ndio maana nikashindwa kukuletea pesa yako, lakini leo sijalala usiku nawaza tu nije nikulipe pesa yako, baada ya kunilipa nikasema kweli sticker inafanya kazi. Na leo nilichelewa kufungua lakini nilikuta wateja wananisubiri foleni, kwa kweli hii sticker msiidharau inafanya kazi, namshukuru sana
Mungu wa Nabii Flora.




SHUHUDA ZA TAREHE 5.FEB.2014

RACHEL ALIYEISHIWA NGUVU MWILI AMSHUKURU MUNGU BAADA YAKUTUMIA STICKER NA SASA NI MZIMA
Bwana Yesu asifiwe, naitwa Reecho; kusema ukweli Mungu wa badhabahu hii siko wa kuchezea, Jumapili nilichukuwa sticker ya pili kwa Nabii Flora, nilipotoka hapa nikamfuata baba Katibu, nikawambia baba nimechelewa kwa sababu toka asubuhi Ibilisi ananifuatilia fuatilia lakini ameshindwa. Nikamwambia nimekosa mafuta ya upako, akaniambia shika kitambaa hiki hapa, nilipofika Mwenge kilichonitokea Mungu mwenyewe anajua, Mungu wa Nabii Flora alinitoa kwenye umauti. Nilipokuwa kwenye daladala nilijisikia miguu imeisha nguvu, hata kunyanyua mkono nilikuwa siwezi. Nilipokuwa kwenye gari nikamwambaia kaka mmoja anitolee maji kwenye pochi yangu, baada ya hapo nikachukuwa hii sticker nikaishika mkononi nikasema Mungu wa Nabii Flora nisaidie hii ni roho ya mauti ishindwe, namshukru Mungu sana kwa kuniokoa.

DADA ANAMSHUKURU MUNGU BAADA YA KUCHUKUWA STICKER YA NABII FLORA NA KWENDA KUIWEKA NYUMBANI KWAKE NA KUOMBA NDUGU YAKE ALIYEKUWA ANAUMWA HAJITAMBUI ALIWEZA KUINUKA, PIA ALICHUWA SABUNI ILIYOOMBEWA NA NABII FLORA BAAYA TU YA KUITUMIA AMEWEZA KUPATA KIBALI KILA SEHEMU

Bwana Yesu asifiwe; mimi ninarafiki yangu anaishi Singida, alikuwa anacheza mpira akapigwa mpira wa kifua, akapelekwa Hospitalini akiwa haongei wala hajitambui. Lakini baada ya kuchukuwa sticker hii na kuibandika chumbani kwangu, nikamuita Mungu wa Nabii Flora, unayeponya, unayeinua naamini hata huyu mtu huko alipo atainuka. Na kweli aliinuka na akaongea na mimi kwa njia ya simu, na hali aliyokuwa nayo ni mbaya. Pia shuhuda mwingine kupitia hizi sabuni zilizoombewa na Nabii Flora, toka nimeitumia hii sabuni nimepata kibali kila sehemu, namshukuru sana Mungu.

DADA BAADA YA KUCHUKUWA STICKER YA NABII FLORA NA KUWEKA NYUMBANI KWAKE HAONI TENA PAKA WAKIMSUMBUA
Bwana Yesu asifiwe; Bwana amenitea kupitia sticker ya Nabii Flora, mimi nyumbani kwangu nilikuwa silali, usiku kuch anakuwa kama nafanyishwa kazi, lakini baada ya kuchukuwa hii sticker na kujweka dirishani kwangu, nimepata muujiza. Siwaoni tena paka dirisshani kwangu na wala hawaji tena nyumbani kwagu.

ANNA MAKINDA ANAMSHUKURU MUNGU WA NABII FLORA KWA KUPATA KIBALI MBELE YA WATU WAKUBWA
Bwana Yesu asifiwe, naitwa Anna Makinda; kuna siku nilikwenda kwenye mkutano wa Serikali, huo mkutano ulikuwa na watu wakubwa, basi wakazungumza watu wote mimi nikawa wa mwisho, nikasema kwa sababu natoka kwenye madhabahu ya Nabii Flora lazima niwe na kibali. Basi wakaniambia nizungumze, cha ajabu mada niliyachangia wote wakaniaunga mkono, na mimi ndio nikachaguliwa, namshukuru sana Mungu wa mahali hapa.

JINSI YA KUFIKA KANISANI

Kama unatokea Mwenge, panda magari ya Tegeta, shuka Mbezi Mbuyuni, uliza kanisani kwa Nabii Flora peter

tembelea
www.nabiiflora.blogspot.com

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...